Saturday, September 28, 2013

Diwani wa Kata ya Katuma Salvatori Msela mwenye shati la mikono mifupi akiongea na wananchi wa Kijiji cha Kapanga  wakiwa na Diwani mwenzake wa Kata ya Mpanda ndogo Mohamed Mapengo mwenye shati la mikono mirefu, wakiongea na wananchi katika kujadili na kupanga mipango ya maendeleo na kuwahimiza wananchi kujitolea nguvu zao  kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati. AKINA MAMA WA KAPANGAWananchi wa Kijiji cha Kapanga wakimsikiliza Diwani wao katika moja ya mikutano ya kuhamasisha uchangiaji wa shughuli za maendeleo Mheshimiwa Diwani hayupo Pichani,Kijiji cha Kapanga kiko Kata ya Katuma Tarafa ya Mwese kwenye nyanda za miunuko ya milima ya mwese, umbali wa  zaidi ya kilometa 75 kutoka Mpanda Mjini  Mkoani KATAVI.
(Picha zote na Kibada Kibada Katavi)
Na     Kibada Kibada –Mpanda Katavi
Wakazi wa Kijiji cha Kapanga kilichopoo Kata ya Katuma Tarafa ya Mwese Wilaya ya Mpanda kinakabiliwa na ukosefu wa Huduma  muhimu za kijamii hali inayowafanya wananchi wa kijiji  kuwahatarini kukubwa na magonjwa ya mlipuko kutokana na kukosa huduma ya maji safi na salama..
Hayo yalielezwa na Diwani wa Kata ya Katuma Salvatory Msela wakati akiongea muda mfupi baada ya ziara kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashuri katika maeneo mbalimbali wilayani humo.
Diwani Msela alizitaja huduma zinazokikabili kijiji hicho ambazo ni  muhimu na wananchi wa Kijiji cha Kapanga wanazokosa kuwa ni huduma ya Maji safia na salama.
 Alieleza kuwa wananchi wa  kijiji hicho hawana huduma  ya maji safi wala salama ,siyo maji ya bomba wala yale ya  kisima na wanategemea maji yanayotiririka kutoka kwenye vijito vilivyopo kijijini hapo maji amabayo siyo rafiki kwa matumizi ya binadamu.
Huduma nyingine wanayokabiliwa nayo ni ukosefu wa huduma ya Afya kwa kuwa kijiji  zahanati,badala yake wanategemea kununua dawa kutoka kwenye vibanda vinavyouza bidhaa za kawaida wanauza   vidonge  aina ya panado ili kutoa huduma kwa wananchi wakazi wa kijiji hicho.
Akifafanua zaidi alieleza kuwa wananchi hao  kutokana na ukosefu wa huduma muhimu za Afya akiwa na maana zahanati na maji hali yao iko hatarini iwapo kutatokea magonjwa ya mlipuko kama kuhara kwa kuwa wanatumia maji ambayo siyo  safi  wala salama ni maji ya mto na asilimia kubwa ni  maji machafu kwa kuwa hata wanyama wanayatumia.
Kuhusu huduma ya Afya wananchi wanalazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilometa kumi  kufuata huduma ya tiba na wanaohangaika zaidi na akina mama na watoto wa  Kijiji cha Kapanga wanaoenda kufuata huduma Katuma makao makuu ya Kata  ilipojengwa  zahanati.
Kufuatia hali hiyo Diwani wa Kata ya Katumba aliomba Serkali kupitia Halmashauri kuweka bajeti  katika mipango  ya maendeleo ya kuwasogezea huduma ya Afya na Maji wananchi hao wa kijiji cha Kapanga ili nao waweze kujisikia kuwa wanafaidi matunda ya nchi kama ilivyo kwa wananchi wenzao wa maeneo mengine.
Akizungumzia shule alieleza kuwa kwa upande wa shule walijitahidi kujenga madarasa ambapo shule ina madarasa japo hayatoshelezi lakini angalau watoto wanasoma tofauti na huduma  ya Afya na Maji.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video