Wednesday, September 25, 2013

SONY DSCWafanyabiashara Ambele Mwasyeba (kulia) na Sebastian Kavishe wanaotuhumiwa kuhujumu Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits kwa kuuza bia ya Windhoek bila ya kuwa na kibali cha kampuni hiyo wakisindikizwa na askari polisi kuingia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo   kusomewa mashtaka yao. Kampuni ya Mabibo ndiyo pekee iliyoruhusiwa kisheria kuingiza na kusamabaza kinywaji hicho hapa nchini
Picha na Philemon Solomon wa Fullshangwe Dar es salaam
WAFANYABIASHARA wawili wakazi wa jijini Dar es Salaam, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka ya kuingilia hakimiliki ya biashara.
Wafanyabiashara hao wanadaiwa kuingilia haki miliki ya kibiashara ya kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Limited ya jijini Dar es Salaam.
Washitakiwa hao Ambere Mwasyeba (38) mkazi wa Mbezi Beach na Sebastian Kavishe (45) mkazi wa Yombo  kwa Abiola, walipandishwa kizimbani Mahakamani leo Septemba 25-2013 na kusomewa mashitaka yao mbele ya Hakimu MKazi Gene Dudu.
Wakili wa Serikali Charles Anindo aliwasomea washitakiwa hao mashitaka yao, ambapo wanadaiwa kuingilia haki miliki ya kibiashara ya kampuni hiyo kwa kufanya biashara ya katoni 1850 za bia aina ya Windhoek  zenye thamani ya Sh milioni 107.3.
Ilidaiwa washitakiwa hao walifanya biashara hiyo bila kuwa na alama halali ya MB66 iliyosajiliwa kwa kampuni hiyo, huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo washitakiwa hao walikana mashitaka yao na kurudishwa rumande baada ya kuzuka mvutano wa kisheria kati ya upande wa mashitaka na upande wa utetezi juu ya dhamana ya washitakiwa. Ambapo upande wa mashitaka ukitaka washitakiwa watoe dhamana ya hati ya mali isiyohamishika ama kuwasilisha nusu ya fedha ya mali hiyo kwa mujibu wa sheria sura ya 148 kipengele (5) kifungu kidogo (e).
Hata hivyo kwa upande wa wakili wa utetezi , Living Kimaro alidai kuwa kosa hilo si fedha kama mali, hivyo hakuna sababu ya wateja wake kutoa nusu ya thamani ya mali hiyo.
Wakili Anindo alidai kwa mujibu wa sheria  haki yoyote iliyothibitishwa kisheria ni mali. Hakimu Dudu aliahirisha kesi hiyo mpaka  itakapokuja kwa ajili ya uamuzi wa dhamana.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video