Ashanti United, Wazee wa kuchezea za uso ligi kuu soka Tanzania bara, toka ligi imeanza hawajaonja ushindi zaidi ya sare moja.
Na Baraka Mpenja , Mbeya
KWA
mara nyingine huenda Ashanti United wakaendelaza rekodi yao mbaya ya
kupanda na kushuka katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara baada
ya leo hii kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Rhino Rangers
Uwanja wa A.H. Mwinyi mjini Tabora.
Mchezp
huo pekee wa ligi kuu ulitarajiwa kuwa wa kufuta makosa kwa Ashanti
kwani tangu waanze ligi kuu wamekuwa wakipokea kichapo kasoro tu
mwishoni mwa wiki walipotoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Azam fc uwanja wa
Azam Complex uliopo maeneo ya Chamazi Mbande nje ya jiji la Dar es
salaam.
Ashanti
ni miongoni mwa timu tatu zilizopanda ligi kuu na inaonekana kuwa
daraja la kuchukulia pointi tafouti na timu za Mbeya City na Rhino
ambazo kwa kiasi kikubwa zimeonesha soka safi na upinzani wa hali ya
juu.
Kipigo
cha leo kinawapa raha zaidi mashabiki wa Rhino waliokuwa na hamu ya
kupata matokeo ya ushindi katika dimba lao la A.H. Mwinyi, lakini kwa
upande wa mashabiki wa Ashanti mambo yanazidi kwenda kombo.
Baada
ya kipigo cha leo, wauza mitumba hao wa Ilala jijini Dar es salaam,
wanarejea katika uwanja wa nyumbani wa Azam Complex jumapili ya wiki hii
kukabiliana na Mtibwa Sugar.
Kutokana
na ubora wa Wana TamTam, Ashanti wanaweza kujikuta wakiambulia kipigo
kingine na kuendelea kujichimbia mkiani mwa ligi hiyo.
Wao
Rhino Rangers watakuwa kibaruani siku ya jumamosi (septemba 28)
kukabiliana na vijana wa Kagera Sugar katika uwanja wao wa nyumbani.
0 comments:
Post a Comment