Wednesday, September 25, 2013

Na Baraka Mpenja, Mbeya
HOMA ya pambano la kukata na shoka baina ya wakali wanaotikisha soka la bongo kwa sasa na kuwafanya mashabiki waumize vichwa juu ya ujio wake, klabu ya Mbeya City dhidi ya Wagosi wa Kaya, Coastal Union katika uwanja wa sokoine jumamosi yazidi kupanda, huku mashabiki wa jiji la Mbeya wakisubiri kuona timu yao ikiwacharaza bakora za moto wapinzani wao.
Kipute hicho kinazidi kutawala katika midomo ya wapenda soka kutokana na ubora wa timu zote mbili, hasa Mbeya City ambao siku za karibuni wamebadili sura ya ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kuonesha upinzani mkali zaidi kwa vigogo Yanga na Simba.
Klabu hii ambayo wachezaji wake hulipwa mishahara na Halmashauri ya jiji, iliibana Yanga Uwanja wa sokoine na kutoka sare ya bao 1-1, huku Yanga wakilalamikia kufanyiwa vurugu na kukata rufaa wakidai mechi ichezwe upya katika uwanja mwingine.
Hapa vijana wa Mbeya City walikuwa wanamuomba Mungu wao kabla ya kuanza kibarua dhidi ya Simba jumamosi ya wiki iliyopita jijini Dar es salaam

Lakini kutokana na kiwango cha Mbeya City watu wengi wanaamini kuwa Yanga walikuwa wanajisafisha mbele ya mashabiki wao kwani walibanwa dakika zote na kukoswa koshwa dakika za lala salama na kama wangezembea hadidhi ingekuwa nyingine.
City waliwashangaza wengi zaidi walipotia maguu yao kwa mara ya kwanza uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dhidi ya Vinara Simba Sc jumamosi ya wiki iliyopita na kutoka sare ya mabao 2-2.
Vijana Walipiga soka la hatari na kuugeuza uwanja mzima kuwa burudani kubwa ya soka, huku mashabiki wengi wakilipuka kwa kushangilia soka maridhawa la vijana hawa na kupelekea mashabiki wa Simba kuomba mpira uishe kwani hali ilikuwa tete na kama zingeongezwa dakika chache, furaha ingeingia shubiri.
Wazee wa Mzuka wanaisubiri mechi ya jumamosi dhidi ya Coatal Union uwanja wa sokoine jijini Mbeya

Kuelekea mchezo wa mwishoni mwa wiki, kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema maandalizi yanaendelea kama kawaida, lakini wao walishajiandaa siku nyingi na sasa kazi yao ni kujiweka sawa kwa kila mechi.
“Tulijiandaa sana kabla ya ligi kuanza, mashindano yameanza, kwa sasa tunatekeleza mipango yetu. Vijana wanashika mafunzo, wapo katika morali kubwa na tunawataka kuongeza bidii zaidi. Tunawaheshimu Coastal, lakini tutakabiliana nao kwa lengo la kusaka ushindi”. Alisema Mwambusi.
Mwambusi aliyejizolea umaarufu na kuwa gumzo kubwa nchini kwa sasa, aliongeza kuwa kwa sasa wamerejea nyumbani baada ya mechi mbili za ugenini ambapo wameambulia pointi 2, kwahiyo mipango yao ni kshinda mechi hiyo muhimu kwao na kujikusania pointi zote tatu kwa mara ya pili tangu kuanza kwa mitanange hiyo.
Aidha aliwataka mashabiki wa soka jijini Mbeya kujitokeza kwa wingi kuwashangilia vijana wao wenye uchu wa kupata matokeo mazuri na kubadili sura ya soka la Tanzania linalotawaliwa na klabu kongwe za Simba na Yanga.
DSC05798 
Kikosi cha Wagosi wa Kaya
Wakati huo huo, jumapili ya wiki hii, Uwanja wa sokoine utahimili daluga za wanaume wawili, Tanzania Prisons “Wajelajela” dhidi ya makamu bingwa wa ligi kuu , Azam fc wenye kumbukumbu ya kuilaza Yanga kwa risasi 3-2 jumapili uwanja wa Taifa.
Prisons wataingia Uwanjani kusaka ushindi wa kwanza baada ya kufungwa mechi mbili za kwanza, na kutoka sare mechi tatu dhidi ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani, Yanga na Mtibwa Sugar katika uwanja wao wa Sokoine.
Mechi nyigine za jumamosi (Septemba 28)  ni kama ifuatavyo;  Yanga vs Ruvu Shooting, Uwanja wa Taifa, Rhino Rangers vs Kagera Sugar, A.H. Mwinyi, na Mgambo JKT Vs JKT Oljoro, Mkwakwani Tanga.
Jumapili (septemba 29 ), JKT Ruvu watakwaruzana na Wekundu wa Msimbazi Simba Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Vibonde Ashanti United watakuwa Azam Complex kuvaana na Mtibwa Sugar, wakati Prisons watakuwa Sokoine kukabiliana na Azam fc.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video