Thursday, September 12, 2013

Na Baraka Mpenja, Mbeya
“MTU akifanya jambo jema, kumpongeza ni haki yake”, leo hii mtandao huu umepata nafasi ya kutembelea uwanja wa kumbukumbu ya hayati Edward Moringe Sokoine jijini hapa na kujionea namna shughuli za ukarabati wa uwanja zinavyoendelea kabla ya mechi kali ya kukata na shoka baina ya wenyeji Mbeya City dhidi ya mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, klabu ya Yanga ya Dar es salaam.
Kwasasa uzio wa uwanja huo unaotenganisha wachezaji wakiwa uwanjani na mashabiki wa majukwaani unaimarishwa  pamoja na dimba lenyewe kuwekwa sawa, na mpaka sasa wapo hatua za mwisho kuzungushia uwanja mzima.
Hakika ni mabadiliko makubwa sana na uzio huu ni mrefu na wakutosha,  waya zote ni mpya, na hii itasaidia kwa asilimia kubwa kuwazuia mashabiki kuingia uwanjani baada ya mechi, labda maaskari wazembee.
IMG-20120915-WA0005 
Siku za nyuma, uzio wa uwanja huu ulikuwa mbaya sana na ilikuwa ngumu sana kuwazuia mashabiki wenye mdadi mkubwa na soka kuingia uwanjani baada ya mechi na kushangilia, hali ambayo ilikuwa hatari sana kwa wachezaji, viongozi wa timu na waandishi wa habari wanaokuwepo kufanya shughuli zao wakati wa mechi.
Lakini kwa sasa hali itakuwa shwari na pongezi kubwa ziwaandee wamiliki wa uwanja, Chama cha Mapinduzi CCM ambapo Meneja Modestus Mwaluka ndiye mwenye dhamana kusimamia uwanja huo.
SAM_0720 
Wakati huo huo, leo hii chama cha soka jijini Mbeya,  MREFA kimetangaza vituo vya uuzaji wa tiketi jijini hapa na baadhi ya vituo hivyo ni Ilomba, Uyole, Iyunga, Kabwe, sokoine uwanjani n.k.
Katibu mkuu wa MREFA, Seleman  Haroub amesema kiingiliao katika mchezo huo ni Tsh.5,000/= na amewatahadharisha watu kununua tiketi maeneo ambayo si maalumu kwani kuna watu wanaweza kuuza tiketi bandia.
“Tunajua wazi kuwa watu wanajipanga kupiga pesa kwenye hii mechi, kwanza tumejipanga kuzuia tiketi bandia kwa kushirikiana na jeshi la polisi. Kiukweli mtu atakayekamatwa na tiketi bandia atakuwa amejitia kwenyae matatizo makubwa sana na atafikishwa mamlaka zinazohusika”. Alisema Haroub.
Haroub amewaonya watu wanaotarajia kutumia mchezo huo kujipatia pesa kwani ulinzi utaimarishwa kila kona na haki itatendeka kwa wale wote wanaofuata taratibu za uwanjani, na wale wakaidi basi rungu litawaangukia.
Katibu huyo amesema mgeni rasmi katika mchezo huo anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Mbeya,  Abas Kandoro na mpaka sasa wanaendelea kuwasiliana na ofisi ya mkuu wa mkoa na hapo kesho watakuwa na kikao ambapo taarifa rasmi itatolewa.
Hata hivyo, Haroub amewaomba wakazi wa Mbeya kujitokeza kwa wingi kushuhudia mechi hiyo na kuishangilia Mbeya City kwani ni timu ya wananchi wote.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video