Meneja
wa Bia ya Castle Lager, Kabula Nshimo na Meneja Mauzo na Usambazaji
Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, James Kavuma wakiongoza maandamano ya
wafanyakazi wa TBL Mbeya kupokea udhamini wa Castle Lager kwa FC
Barcelona katika mitaa ya jiji la Mbeya mwishoni mwa wiki
Bendi ya Magereza Mbeya ikiongoza maandamano ya wafanyakazi wa TBL Mbeya kupokea udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona
Bodaboda wakiwa katika shangwe za maandamano ya wafanyakazi wa TBL Mbeya kupokea udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona Wafanyakazi wa TBL Mbeya wakicheza kwaito kusherekea udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona Wafanyakazi wa TBL Mbeya wakicheza foosball kusherekea udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona Kikundi cha sanaa cha Bombeso wakitoa burudani
Wananchi wa jiji la Mbeya wakitazama maandamano ya wafanyakazi wa TBL Mbeya kupokea udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona Wafanyakazi wa TBL Mbeya wakicheza mduara kusherekea udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona
…………..
Na Mwandishi Wetu
Wafanyakazi
wa Kampuni ya Bia Tanzania kiwanda cha Mbeya wamehitimisha shamrashamra
za kupokea udhamini wa Castle Lager kwa FC Barcelona zilizodumu kwa
mwezi mmoja nchi nzima. Kama ilivyokuwa maeneo mengine, maelfu ya
mashabiki wa soka jijini Mbeya pia wamepata fursa ya kuwa sehemu ya
shamrashamra hizo zilizofanyika mwishoni mwa wiki na kuvutia maelfu ya
mashabiki wa kandanda.
Shamrashamra
hizo zilihusisha maandamano makubwa ya wafanyakazi wa Kampuni Bia
Tanzania (TBL) pamoja na vikundi vya sanaa vya Magereza Brass Band na
Bombeso waliokatiza katika mitaa ya jiji la Mbeya wakitoa burudani ya
muziki, matarumbeta na manjonjo ya kucheza kandanda.
Wakati
wa maandamano hayo mashabiki wengi wa mpira wa miguu walijitokeza
barabarani kushuhudia utambulisho huo, baadhi yao wakiwa wamevalia jezi
za Barcelona.
Maandamano
hayo yaliyowahusisha wafanyakazi wa TBL yalianzia katikati ya jiji la
Mbeya na kupita katika mitaa kadhaa ya katikati ya jiji la Mbeya na
kuishia Iyunga kilipo kiwanda cha TBL yakiwa na lengo la kuutambulisha
ubia wa Castle Lager na Barcelona kwa wafanyakazi wa TBL pamoja na wadau
wa michezo wa Mbeya.
Pia
maandamano hayo yalikuwa na lengo la kuonyesha sapoti ya wafanyakazi hao
kwa ubia wa Castle Lager na FC Barcelona, ambayo inatajwa kuwa ni klabu
ya karne kutokana na mafanikio makubwa na kuwa na wapenzi wengi zaidi
duniani kuliko timu nyingine yoyote.
Wakati
wa maandamano hayo mashabiki wengi wa mpira wa miguu walijitokeza
barabarani kushuhudia utambulisho huo, baadhi yao wakiwa wamevalia jezi
za Barcelona.
Akizungumza
na wafanyakazi wa TBL katika hafla iliyofanyika kwenye kiwanda cha TBL
Mbeya kuhusu ubia wao na Barcelona, Meneja Mauzo na Usambazaji wa Kanda
ya Nyanda za Juu Kusini wa TBL, James Kavuma amesema wafanyakazi wa TBL
Mbeya na wananchi wa Mbeya wameupokea udhamini huo kwa furaha kwani
anaamini kuwa udhamini huo utaweka karibu mashabiki wa Barcelona na
klabu yao waipendayo kupitia bia ya Castle Lager.
‘’Udhamini
huu umelenga mambo mengi, moja ikiwa ni kuwaweka karibu wapenzi wa
klabu hiyo waliopo Tanzania na Barcelona. Lakini si hilo tu, yapo mambo
mengi yenye manufaa kwa jamii yatakayopatikana kutokana na udhamini huo
wa miaka mitatu.’’
Naye
Meneja Mauzo wa Kanda hiyo, Michael Myinga alisema kuwa kutokana na
historia ya zaidi ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa FC Barcelona na
Castle Lager basi ubia huu unaleta maana kubwa na ni muafaka ukizingatia
kuwa Castle Lager ni kinywaji cha bara zima la Afrika.
Meneja
wa Castle Lager Kabula Nshimo alisema kwamba sherehe hizo zilizofanyika
Mbeya ndio za mwisho katika mlolongo wa kuzindua mahali pote ambapo TBL
ina viwanda. Aliongeza kuwa sasa shughuli nyingine mbalimbali
zinazohusisha wadau wa soka na jamii kwa ujumla ndio zitakazofuatia
kupitia shughuli mbalimbali zilizopangwa kufanyika nchi nzima katika.
0 comments:
Post a Comment