Thursday, September 26, 2013

Taswa_Fc 
Na Mwandishi wetu
TIMU ya soka ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa FC) kesho (Ijumaa) itacheza mchezo maalum wa kirafiki dhidi ya timu ya kombaini ya Shirikisho la Kandanda la Tanzania (TFF) na Chama cha soka cha mkoa wa Dar es salaam (DRFA).
Mchezo huo umepangwa kuanza saa 10.00 jioni kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume na TFF itaongozwa na Katibu wake mkuu, Angetile Osiah, Boniface Wambura (Msemaji), Saad Kawemba, Sabri na kipa, mzee Mshangama.
Mbali ya wachezaji timu hiyo itakuwa na viongozi wengine wa DRFA akiwemo, Msanifu Kondo, Almasi  Kasongo, Mohamed Mharizo. Pia kocha mkuu wa timu ya Taifa, Kim Poulsen, kocha wa timu za vijana, Jacob Michelsen na wasaidizi wao kama Jamhuri Kihwelu, Peter Manyika na wengineo watakuwepo uwanjani.
Mwenyekiti wa Taswa FC, Majuto Omary alisema kuwa mbali ya yeye kuongoza jahazi la timu yake, pia watakuwepo wachezaji wengine kama Ali Mkogwe, Juma Pinto, Wilbert Molandi, Sultan Sikilo, Salum Jaba, Deogratius “Super Deo” Maganga, Kelvin Kiwia, Julius Kihampa, Sweetbert Lukonge, Elius Kambili, Zahoro Mlanzi, Frank Balile, Mwarami Seif, Saidi Seif na wengine wengi.
“Huu ni mchezo wa kudumisha ushirikiano wetu kwani sisi ni waandishi wa habari za michezo na wao ni miongoni mwa wadau wetu, hivyo nawaomba wachezaji wote wafike kwa wingi ili kuona mechi hiyo ya aina yake,” alisema Majuto.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video