Wednesday, September 18, 2013


Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
HATIMAYE mzunguko wa nne wa ligi kuu soka Tanzania bara umeendelea kushika kasi leo hii kwa timu zote 14 kushuka dimbani katika viwanja saba tofauti nchini.
Wekundu wa Msimbazi , Simba SC “Taifa Kubwa” chini ya kocha Abdallah Kibaden `King Mputa` wamewakaribisha wapigwa kwata wa Mgambo Sooting Stars wanaonolewa na kocha Ramadhan Kampira kutoka jijini Tanga `Waja leo waondoka leo`  katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam na kushuhudia dakika 90 za kipute hicho zikimalizika kwa Mnyama kushinda mabao 6-0, huku Mrundi Amis Tambwe akipiga manne peke yake.
Tambwe ambaye alipondwa hivi karibuni kwa kutofunga mabao aliandika mabao yake katika dakika ya 4, 42, 44, 88.
Kwa matokeo hayo, Mnyama amefikisha pointi 10 na kukaa kileleni mwa ligi hiyo.
Mabao mengine ya Simba yamefungwa na Mtanzania kinda mwenye kasi kubwa na ujuzi wa hali ya juu, Haroun Chonongo katika dakika ya 32 na 64.
DSC_0168 
Huko jijini Mbeya `Jiji la kijani`, mabingwa wa ligi hiyo, klabu ya Yanga ya Dar es salaam chini ya kocha Mhlolanzi, Ernie Brandts, kwa mara nyingine tena wameshuka katika dimba la kumbukumbu ya Sokoine kuwakabili maafande wa Tanzania Prisons `Wajelajela` na kushuhudia dakika tisini zikimalizika kwa sare ya 1-1.
Bao la kwanza la Yanga limefungwa katika dakika ya 41 kufuatia mpira mrefu uliorushwa na Mbuyu Twite na kumkuta Simon Msuva ambaye alitoa  pande kwa Jerry John Tegete aliyezamisha mpira kimiani.
Prisons walisawazisha bao hilo kupitia kwa Fredy Chudu katika dakika ya 77 na kusababisha mabingwa Yanga kuvuna pointi 2 tu katika mechi mbili za Mbeya na hatimaye kufikisha alama 6 kibindoni.
YANGA WAKISHANGILIA 
Nao Makamu bingwa wa ligi hiyo, matajiri wenye jeuri ya pesa, wana lambalamba, Azam fc wameoneshana kazi na wageni wa ligi kuu wenye historia ya kupanda na kushuka, Ashanti United `Watoto wa jiji` na kushuhudia dakika zote zikimalizika kwa sare ya 1-1 na kumfanya kocha Sterwat John Hall azidi kupasuka kichwa.
Dimba la CCM Mkwakwani jijini Tanga limehimili daluga za wenyeji Coastal Union `Wagosi wa Kaya” dhidi ya Rhino Rangers,ambapo mchezo huo umemalizika kwa sare ya bao 1-1.
AzamFC 
Kagera Sugar walikuwa katika dimba lao la Kaitaba kuikabili JKT Oljoro na kushuhudia vijana wa Jackson Mayanja aliyerithi mikoba ya Kibadeni wakiwabamiza Oljoro mabao 2-1.
Mechi nyingine ilikuwa huko dimba la Manungu Complex ambapo wana TamTam, Mtibwa Sugar wamewakaribisha Mbeya City chini ya kocha Juma Mwambusi na dakika tisini zimemalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana (0-0).
Mchezo huo ulikuwa wa kwanza kwa Mbeya City kucheza nje ya uwanja wa nyumbani, hivyo ni matokeo mazuri kwao kwani pointi moja si haba ugenini.
Huko Uwanja wa Mabatini Mlandizi mkoani Pwani, wanandugu wawili, Ruvu Shooting wamewakaribisha JKT Ruvu na kushuhudia soka la upinzani mkubwa, lakini dakika zote zimemalizika kwa matokeo ya Charles Mkwasa na kikosi chake kuwafumua JKT Ruvu kwa bao 1-0 na hivyo kushushwa rasmi kileleni ambapo sasa Simba wameanza kubarizi baada ya kushusha mvua katika mchezo wa leo dhidi ya Mgambo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video