Sunday, September 29, 2013


Na Baraka Mpenja, Mbeya
Ligi kuu soka Tanzania bara inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mechi tatu kupigwa ambapo mechi inayowavutia mashabiki wengi wa kabumbu ni baina ya vinara wa ligi hiyo, Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc dhidi ya wenyeji wao katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam jioni ya leo, Maafande wa JKT Ruvu.
JKT Ruvu wataingia uwanjani wakiwa tayari wameporomoshwa hadi nafasi ya nne wakiwa na pointi 9 na katika nafasi ya tatu baaada ya matokeo ya jana Uwanja wa Sokoine, Coastal Union “Wagosi wa Kaya” wanakalia kwa pointi 10 wakitokea nafasi ya tano, huku nafasi ya pili ikishikiliwa na Kagera Sugar waliofikisha pointi 11 sawa na Simba lakini wanatofautiana kwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Wataweza leo?: Mechi iliyopita Simba walitulizwa kwa sare ya 2-2 na Mbeya City na pichani ndivyo walitoka Uwanjani Vichwa chini, na leo hii watakula sahani moja na JKT Ruvu, je, Amis Tambwe kuendeleza ufundi wa kufumania nyavu?

Mechi hii ina mvuto wa aina yake kutokana na watani wa jadi wa Simba, klabu Yanga kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting jana ukiwa ni ushindi wa kwanza katik  mechi tano walizoshuka dimbani.
Kwa kawaida matokeo ya wanajangwani yataongeza ladha ya mchezo wa leo kwani Simba watahitaji kushinda ili kuendelea kukalia usukani wa ligi hiyo na kuwafanya Yanga wazidi kuisoma namba Kibadeni..
Pia kuwa fiti wa Warundi, Gilbert Kaze na Amisi Tambwe kumeongeza hamu ya mashabiki kuwaona wanandinga hao wakiendelea kung`ara, hususani Tambwe ambaye anaoongozwa kwa kupachika mabao mpaka sasa akiwa nayo 6 katika mechi mbili tu.
9 
Nyomi yote hii iko nyuma ya Simba sc

Aidha katika mechi hiyo, makocha wazalendo wanakutana kuanzia makocha wakuu hadi wasaidizi, Abdallah Athuman Seif “King Kibadeni” na Jamhuri Kiwhelo `Julio` kwa Simba, huku JKT Ruvu ikiongozwa na Mbwana Makata pamoja na Greyson Haule.
Maarifa ya wabongo hawa yatapimana leo uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam na endapo Simba watashinda leo, watajikita zaidi kileleni wakifikisha pointi 14 na kama Ruvu Watashinda watapanda juu zaidi kwa kujikusanyia pointi 12 kileleni, lakini itategemeana kwani Azam wakishinda pia watafikisha pointi 12 na hapo hesabu ya mabao itatumika.
Majembe: Azam FC nao wanasubiri balaa lao kutoka kwa Prisons leo


Uwanja wa Sokoine kwa siku ya pili mfululizo utahimili daluga za Maafande wa jeshi la Magereza Tanzania, Prisons ya Mbeya dhidi ya wana Lambalamba wa Azam fc kutoka jijini Dar es salaam.
Tayaru timu zote zimeshatambiana kuelekea mtanange huo ambapo katibu mkuu wa Prisons, Inspekta, Sadick Jumbe ametamba kuwa klabu yake imejiandaa vizuri kuvuna mtaji wa pointi tatu na vijana wake wako katika morali kubwa.
Wakati kwa upande wa Azam fc kupitia kwa Afisa habari wake, Jafar Idd Maganga wamekiri ugumu wa mechi ya leo, hasa kutokana na ukomavu wa wapinzani wao, lakini nia yao ni kushinda na kuchukua pointi tatu muhimu.
TFF Tanzania Prisons 
Mtawapigisha kwata Azam?: Prisons wana kibarua kizito leo uwanja wao wa sokoine jijini Mbeya

Mbali na kipute hicho, vibonde  wa ligi hiyo na uchochoro wa kuchukulia pointi Msimu huu, klabu ya Ashanti United inaikaribisha Mtibwa Sugar katika uwanja wa nyumbani wa Azam Complex, mbande Chamazi, nje kidogo ya jijini la Dar es salaam. 
Kama waburuza mkia hao watashinda leo, halafu Prisons akafungwa, wajelajela wataisoma namba mkiani, lakini kama Ashanti watashinda na na Prisons wakishinda, wataendelea kuburuza mkia. 
Kwasasa Ashanti wanavuta mkia wakiwa na pointi moja tu katika mechi 6 walizocheza. Wamefungwa tano na kutoa sare moja na Azam fc.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video