BAADA
ya kukabidhi nyumba kwa wanachama 38, Mtandao wa wasanii Tanzania
(SHIWATA) unatoa shukurani kwa viongozi wa kijiji cha Mwanzega Kata ya
Mbezi, Tarafa ya Shungubweni,wanavijiji pamoja na viongozi wa wilaya ya
Mkuranga akiwepo Mkuu wa wilaya, Mercy Silla kwa kufanisha sherehe ya
ugawaji nyumba na vyeti.
Wanachama
zaidi ya 70 wamejitokeza kuchangia ujenzi wa nyumba ili wakabidhiwe
Desemba 28, 2013 katika sherehe nyingine ya kukabidhi nyumba ambayo
inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali ambao waliomba udhuru
sherehe ya awali.
SHIWATA
inawahimiza wanachama wake wasifanye mzaha na kudharau mpango wa
kuchangia ujenzi kwani utawanufaish na kuwamilikisha nyumba zao wenyewe
kwa gharama nafuu.
Mtandao
wa wasanii unatoa bure viwanja baada ya mwanachama kulipa gharama zote
za kujiunga uanachama ambaye ataruhusiwa kujenga mwenyewe au kuchangia
ujenzi wa nyumba kwa pamoja.
SHIWATA
inakusudia kujenga Shule ya Msingi, Sekondari na vyuo vya fani za
utamaduni, Uandishi wa Habari na michezo mbalimbali ikiwemo soka kwa
malengo ya kupata wachezaji bora ambao watanyanyua viwango vya michezo
hiyo ndani na nje ya nchi ili kuwapatia vipato zaidi.
Pia
inawahitaji wasanii, wanamichezo, wanahabari wenye vipaji na elimu ya
juu katika fani zao wajiunge na SHIWATA ili waweze kuwa walimu wa sanaa
na michezo mbalimbali ambayo itaanza kufundishwa kutoka ngazi ya Shule
ya Msingi, Sekondari hadi Chuo katika kijiji cha Mwanzega.
Shule
ya msingi itakapoanzishwa itatoa kipaumbele kwa masomo ya sanaa na
michezo ili kupata wasanii na wanamichezo bora katika taifa letu.
SHIWATA
pia inatarajia kujenga viwanja vya michezo, kumbi za Maonesho na Studio
za kurekodia muziki na filamu zenye ubora ambazo zitauzwa ndani na nje
ya nchi.
0 comments:
Post a Comment