Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof.
Elisante Ole Gabriel (kushoto) akimkaribisha Bondia Mstaafu Rashid
Matumla (kulia) leo alipowasili ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari , Vijana , Utamaduni na Michezo(WHVUM)
Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akiongea na Bondia Mstaafu Rashid
Matumla (Snakeman) alipomtembelea leo ofisini kwake jijini Dar es
Salaam.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo , Prof.
Elisnate Ole Gabriel, (kulia) akiongea na Bondia Mstaafu Rashid
Matumla(wenye fulana ya mistari) leo jijini Dar es Salaam, ambapo
ametakiwa kurithisha kipaji chake kwa vijana nchini (kushoto) ni
Mkurugenzi wa Michezo katika wizara hiyo Leonard Thadeo.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof.
Elisante Ole Gabriel (kulia) pamoja na Bondia Mstaafu Rashid Matumla
(mwenye fulana ya mistari ) wakimsikiliza Mkurugenzi wa Michezo katika
Wizara hiyo Leonard Thadeo(kushoto) wakati akitoa maelezo leo jijini Dar
es Salaam ,
Picha
ya pamoja – Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye miwani) Mkurugenzi wa
Michezo katika wizara hiyo Leonard Thadeo( mwenye koti jeusi kulia),
Bondia Mstaafu Rashid Matumla (mwenye fulana ya mistari)), pamoja na
Afisa Vijana katika wizara , Amina Sanga(kushoto).
Picha zote na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO
Na Concilia Niyibitanga
Wizara ya Hbari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Serikali
kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imemtaka Bw.
Rashid Matumla ambaye ni bondia mstaafu katika mchezo wa ngumi za ridhaa
kurithisha kipaji chake kwa vijana wengine.
Hayo
yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Prof Elisante Ole Gabriel wakati
akiongea na Bw. Matumla alipomtembelea ofisi kwake.
Prof.
Gabriel amemtaka kuanzisha kikundi cha vijana ambacho ataweza
kukifundisha mchezo huo ili kipaji chake kisipotee ukizingatia kuwa
Tanzania ina wachezaji wachache katika mchezo huo.
“Ni
vema ukarithisha ujuzi wako katika mchezo wa ngumi kwa vijana chipukizi
kwa kuwafundisha na kuwashauri katika mchezo huo” Amesema Prof.
Gabriel.
Amesema
kuwa Serikali inatambua mchango wake katika mchezo wa ngumi hapa nchini
na hivyo si vema akakaa na ujuzi wake ukizingatia kuwa yeye amestaafu
katika mchezo huo.
Aidha,
Prof. Gabriel ameongeza kuwa kwa kufanya hivo Matumla atawasaidia
vijana chipukizi kuwa Mabondia wazuri wa baade ikiwa ni pamoja na
kujiajiri badala ya kujihusisha na vitendo vibaya kama matumizi ya
madawa ya kulevya n.k
Naye
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Bw. Leonard Thadeo amesema kuwa
kikundi hicho kinaweza pia kikajihusisha na ujasiriamali kwa kuomba
mikopo katika Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa kuwa wanamichezo pia
wanatakiwa kujishughulisha na ujasiriamali ili kujiongezea kipato.
Kwa
upande wake Bw. Matumla amesema kuwa amefurahi na amefarijika sana
kuongea na viongozi wa wizara inayosimamia michezo na vijana kwa kuwa
wameonesha kutambua mchango alioliletea Taifa hili katika mchezo huo.
Matumla
amesema kuwa atafanya kila awezalo kuhakikisha kuwa anawarithisha
mabondia chipukizi na vijana wengine kipaji chake katika mchezo huo ili
wawe mabondia bora wa baadaye.
0 comments:
Post a Comment