MSHAMBULIAJI
wa Timu ya Taifa ya England maarufu kwa jina la `simba watatu` na klabu
ya Liverpool, Daniel Sturridge atakaa nje ya dimba katika kipute cha
kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia keshokutwa jumanne dhidi ya
Ukraine mjini Kiev.
Sturridge
alikosa mechi ya ijumaa usiku dhidi ya Moldova katika dimba la Wembley
baada ya kupata maumivu ya mguu wake katika mechi kali ya ligi kuu soka
nchini England baina ya Liverpool dhidi ya Manchester United mwishoni
mwa wiki iliyopita.
Ilitumainiwa
kuwa mshambuliaji huyo angepona mapema na kurudi uwanjani leo jioni,
lakini taarifa za madaktaria zinasema hawezi hata kidogo.
Janga: Daniel Sturridge atakaa nje ya kikosi cha England dhidi ya Ukraine kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia mwakani
Japokuwa chama cha soka cha England, FA hakijathibitisha kama jambo hilo litatokea.
‘ FA
inaweza kuthibitisha kuwa Daniel Sturridge hatarudi uwanjani katika
kikosi cha England kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia dhidi ya
Ukraine jumanne,” Ilisema taarifa ya FA.
‘Timu
ya madaktari wa England imekuwa ikiwasiliana na matabibu wa Liverpool
tangu arejea huko alhamisi, afya yake inaimarika, lakini haijulikani
kama Sturridge atakuwa sawa katika mechi Kiev jumanne jioni.’
Balaa
safu ya ushambuliaji: Danny Welbeck hatacheza mechi dhidi ya Ukraine
baada ya kuoneshwa kadi ya njano wakati wa mechi na Moldova
Acha hizo wee jamaa!: Roy Hodgson alichukizwa na kumlalamikia mwamuzi baada ya kutoa kadi ya njano kwa Welbeck
0 comments:
Post a Comment