Rais
na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akivishwa skafu kutoka kwa chipukizi mara tu baada ya kuingia wilayani
Sengerema kwa ziara ya siku moja tarehe 10.9.2013.
Rais
Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Katunguru
kilichoko wilayani Sengerema alipokwenda kijijini hapo kwa kwa ajili ya
kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Katunguru/ Nyamtelela
tarehe 10.9.2013.
Rais
Dkt. Jakaya Kikwete akiweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa
Katungulu/Nyamtelela utakaogharimu shs milioni 734 na utawanufaisha
zaidi ya watu elfu kumi.
Rais
Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Luchili akiwa
njiani kwenda katika kijiji cha Bukokwa kuzindua rasmi mradi wa umeme
tarehe 10.9.2013.
Wageni
waalikwa wakifuatilia kwa makini sherehe za uzinduzi wa mradi wa umeme
vijijini uliofanywa na Rais Kikwete huko Bukokwa wilayani Sengerema
tarehe 10.9.2013.
Waziri
wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipokea hati ya
makabidhiano ya mradi wa umeme wa Bukokwa uliofadhiliwa na Millenium
Challenge Co-operation ya Marekani.
Rais Jakaya Kikwete akiangalia michoro inayoonyesha usambazaji wa umeme katika mkoa wa Mwanza. Rais Dkt. Jakaya Kikwete akizindua rasmi mradi wa umeme wa Bukokwa tarehe 10.9.2013
PICHA NA JOHN LUKUWI
0 comments:
Post a Comment