Monday, September 16, 2013


TFF Tanzania Prisons 
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
MAAFANDE wa jeshi la Magereza, Tanzania Prisons “Wajelajela” wamewaomba mashabiki wa jiji la Mbeya kujitokeza kwa wingi kuwapa hamasa katika mchezo wao mkali na wakukata na shoka wa ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Mabingwa watetezi, klabu ya Yanga, keshokutwa uwanja wa sokoine Mbeya.
Akizungumza kwa njia ya simu na mtandao wa FULLSHANGWE, katibu mkuu wa Tanzania Prisons, Inspecta Sadick Jumbe amesema wanajua wazi Mbeya ina watu wengi wanaopenda soka, na ndio maana walijitokeza kwa wingi zaidi katika mchezo wa ndugu zao Mbeya City dhidi ya Yanga, hivyo wajitokeze hata mwenye mchezo wao.
“Mbeya City ilishangiliwa na umati mkubwa wa watu, mashabiki waje na kwenye mchezo wetu dhidi ya Yanga ili tuwe pamoja kusaka ushindi wa kwanza katika mchezo wa kwanza uwanja wa nyumbani”. Alisema Jumbe.
Jumbe alisema wameanza ligi kwa mechi tatu za ugenini, hakika ilikuwa kazi ngumu sana kwao na sasa wanarejea nyumbani kucheza mechi ngumu zaidi na mabingwa watetezi, lakini wamejiandaa kushindana kwa nguvu zote ili kupata matokeo ya ushindi.
“Yanga ni timu bora na ndio mabingwa watetezi, wana wachezaji wazuri, lakini mwaka jana tulitoka nao suluhu uwanja wa Sokoine na walitufunga Dar es salaam, mwaka huu tunaanza nao tena nyumbani, hakika tutakomaa vibaya sana na kufuta matokeo mabaya ya awali”. Alisema Jumbe.
Katibu huyo alisema mashabiki wameanza kupoteza imani na kikosicha Jumanne Chale na kuamini kuwa huenda kikafanya vibaya zaidi msimu huu, lakini amewaondoa shaka kuwa ligi bado ni mbichi na timu inazidi kuimarika kuanzia mchezo dhidi ya Coastal Union jumamosi.
“Mechi ya Coastal tulikuwa na uwezo wa kushinda mabao matatu, lakini nao waamuzi walichangia kutunyima ushindi, tulinyimwa penati za wazi na goli moja tulilozamisha nyavuni, lakini yote kwa yote mwamuzi ndio mtu wa mwisho, tulikubali na sasa tunasonga mbele.”. Alisema Jumbe.
Kwa sasa Tanzania Prisons wapo nafasi ya pili toka mkoani kwa kujikusanyia pointi moja tu katika mechi tatu za kwanza.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video