Saturday, September 28, 2013


Kim Poulsen 
Mahmoud Ahmad Arusha
Kocha mkuu wa timu ya taifa(TAIFA STARS)Kim Poulsen amesema kuwa msingi mzuri wa timu ya taifa unaanzia kwa vijana kupewa mafunzo ya soka angali wakiwa bado wadogo na kupata makocha wenye utaalamu wa soka kuwafundisha soka vijana hao iliwaje kuwa mabalozi wazuri wa timu ya taifa kwa siku za usoni.
Poulsen amesema hayo jijini hapa leo wakati alipokuwa balozi wa heshima kwenye uzinduzi wa ligi ya Moivaro youth kwenye viwanja vya shule ya kimataifa ya moshi iliyopo nje kidogo ya jiji la Arusha na kutanabaisha kuwa ligi hiyo ni njia sahihi ya kupata wachezaji wa timu ya taifa kwa kuwa kituo hicho kinachoendesha ligi hiyo kimekuwa kikifundisha kozi za awali na kati kwa walimu wa soka na hiyo ni misingi imara ya soka.
Akawataka wadau mbalimbali hapa nchini kuiga mfano huo katika juhudi za kukuza soka la vijana kwa kutoa misaada ya vifaa na fedha za uendeshaji wa soka hilo ilikukuza vipaji lukuki vilivyopo hapa nchi ilikujenga msingi imara wakuwa na timu ya taifa hapo usoni itakayokuwa imeandaliwa kiutaalamu tokea chini hadi timu ya taifa.
“unajua hapa nimeona vijana wawili watakao kuwa msaada kwa timu ya vijana kama watapewa mafunzo ya kiutaalam na ninaamini kuwa kwa makocha niliowaona hapa hilo linawezekana ili klabu hii imenifurahyisha na kunitia moyo kuwa msingi wa soka na vifaa wanavyopewa vijana vinaonyesha vipo kitaalamu na vitasaidia ujenzi wa soka la kisasa kwa wachezaji hawa wa siku za usoni”alisema Kim
Nae Mkurugenzi wa Future Stars Alfed Itael amesema kuwa ligi hiyo itaendeshwa kwa nyumbani na ugenini na timu zaidi ya 30 zinashiriki mashindano hayo na kubainisha kuwa ligi hiyo itadumu kwa kipindi cha kuanzia leo hadi mwezi wa March mwakani atakapopatikana Bingwa wa ligi hiyo.
Itael alisema kuwa ujio wa kocha mkuu wa taifa stars ni muendelezo wa kuwapa changamoto vijana wanaoshiriki ligi hiyo kupata hamasa ya kujua majukumu yao uwanjani kwani soka ni sehemu ya ajira kwa vijana hao kujituma iliwaandae msingi wa soka lao siku za baadae akawataka vijana kuitumia ligi hiyo kuweza kuweka msingi wa soka la kisasa kwa kufuata maagizo ya walimu wao.
Ligi hiyo pia ilizikutanisha timu za New Vision na FutureStars akatika mechi ya ufunguzi na timu ya future stars kuibugiza new vision kwa mabao matatu kwa nunge katika mtanange wa kukata na shoka uliopigwa baada ya ufunguzi wa ligi hiyo iliyoonyesha ushundani kwa timu mbali mbali zilizopata kushiriki siku ya leo.
Akizungumza baada ya mechi hiyo mmoja wa vijana mwenye umri wa miaka 13 Yasin Hashimu wa timu ya New Vision alisema kuwa mashindano hayo ni mazuri na yatamsaidia kufikia malengo yake ya kuwa machezaji wa kimataifa kwa siku za usoni na kuwa kufungwa kwa ni sehemu ya mchezo na wanaenda kujipanga kuhakikisha mechi inayofuata wanatoa upinzani kwa timu watakayokutana nayo.
Hashimu akawataka wachezaji wenzake kufuta ushauri na mafunzo wanayopewa na walimu wao ilikuwa wachezaji tegemeo kwa timu zao hapo baadae kwani soka ni ajira na inajenga miili yetu na kutoa burudani kwa watazamaji kokote ulimwenguni.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video