Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
MCHEZAJI ghali zaidi Duniani, Gareth Bale hajagusa hata nyasi za Bernabeu baada ya kuvunja rekodi ya Dunia ya usajili kwa dau la pauni milioni 86, lakini shida zimeshaanza katika chumba cha kubadilishia nguo katika klabu ya Real Madrid.
Thamani ya Mesut Ozil kwa wachezaji wenzake wa Real Madrid ilionekana jumatano jana wakati wachezaji walikuwa wanapiga kelele za kumkubali huku wakisema haina shida Bale atarithi mikoba yake.
Kwa upande wa nyota wa Ureno na klabu hiyo, Cristiano Ronaldo amenyong`onyea baada ya kumpoteza Ozil, wakati huo huo nao Alvaro Arbeloa, Isco na hata nyota wa wapinzani wao, FC Barcelona, Cesc Fabregas wamekerwa na kitendo cha Mjerumani huyo mwenye kipaji cha juu kuondoka ligi ya Hispania.
Hasira: Cristiano Ronaldo ameripotiwa akilaumu mbele ya wanandinga wenzake wa timu ya taifa ya Ureno kuwa amechukizwa na kuuzwa kwa Mesut Ozil
Akiongoza mazoezi: Ronaldo, akifanya mazoezi na timu ya taifa ya Ureno, na ana amini Ozil alikuwa mpikaji mzuri wa pasi wanapokuwa dimbani
Katika majadiliano? Ronaldo akitembea kutokea mazoezi ya timu ya Taifa ya Ureno akiwa na mchezaji mwenzake wa Real Madrid Pepe (kulia)
Anamkubali: Kiungo mshambuliaji wa Real Madrid, Isco anamkubali sana Ozil
Akiwa kazini: Lakini kwasasa Ozil yuko Arsenal na kuondoka kwake kumewahuzunisha wachezaji nyota wa Real Madrid
0 comments:
Post a Comment