Tuesday, September 24, 2013

b433968b4b2ce9be8d4855c2bf09c03f_XLMwakilishi wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia ametaka kuzidishwe mapambano dhidi ya kundi la kigaidi la ash-Shabab.
Nicholas Kay ameyasema hayo leo katika kikao na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswis na kuitaka jamii ya kimataifa izidishe juhudi za kupambana na kundi hilo. Amesema kuwa hadi sasa serikali ya Somalia imeweza kwa kiasi fulani kurejesha hali ya usalama katika maeneo mengi ya nchi hiyo na akaongeza kuwa, pamoja na hayo bado kuna haja ya kuisaidia nchi hiyo kwani serikali ya Mogadishu bado inakabiliwa na kundi hilo.
Kay amesema shambulizi lililofanywa na wapiganaji wa al Shabab dhidi ya jengo la kibiashara huko mjini Nairobi, Kenya sio la kushangaza, kwani ni miongoni mwa jinai kubwa ambazo zimekuwa zikitekelezwa na kundi hilo. Amesema kuwa, usalama wa Somalia unategemea kusambaratisha kwa kundi hilo la ash-Shabab.
Wakati huo huo Waziri Mkuu wa Somalia  Abdi Farah Shirdon ameiomba jamii ya kimataifa kusaidia juhudi za kuliangamiza kundi la kigaidi la al Shabab ambalo limetangaza kwua ndilo lililotekeleza shambulizi dhidi ya jumba la maduka la Westgate jijini Nairobi.
CHANZO: RADIO TEHRAN

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video