Friday, September 27, 2013

DSC_0129 
Pichani: Mheshimiwa Dk. Migiro akiwa katika  picha ya pamoja na maafisa  wa Ubalozi. Kutoka kushoto ni Amos Msanjila, Allen Kuzilwa, Rose Henry Kiondo, Wema Kibona, Idris Zahran, Caroline Kitana Chipeta na Yusuf Kashangwa. 
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa NEC wa Siasa na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Dk. Asha-Rose Migiro  atembelea Ubalozi wa Tanzania hapa London, kwa lengo la kuwasabahi maafisa wa Ubalozi na kuwapatia taarifa mbalimbali za maendeleo ya ushiirikiano na vyama marafiki na CCM, hususan Chama cha Labour cha Uingereza.
Mhe. Dk. Migiro alipita Ubalozini akitokea mji wa Brighton,  Kusini mwa Uingereza alikokuwa akihudhuria Mkutano Mkuu wa wa Chama cha Labour uliofanyika huko kuanzia tarehe 22 hadi 25 Septemba 2013. Katika mazungumzo yake na maafisa  hao Dk. Migiro aliwadokeza   kuwa akiwa Brighton alifanikiwa kukutana na kuanzisha mawasiliano na maafisa mbalimbali wa Chama cha Labour kwa lengo la kuimarisha zaidi ushirikiano wa vyama vyao.  

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video