Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
BEKI
nyota wa Asernal, Mjerumani, Per Mertesacker amemsifia kocha wake
Arsene Wenger kunasa jembe la ukweli, Mesut Ozil kutoka Real Madridi
licha ya kutumia fedha nyingi zilizovunja rekodi ya klabu yake.
Wenger alitumia dau la pauni milioni 42.5 kwa nyota huyo wa Ujerumani na kuvunja rekodi ya klabu ya Arsenal akiwa kocha mkuu.
Lakini, Mertesacker, amesema Ozil wanayecheza pamoja timu ya taifa atafanya makubwa na kufanikiwa kisoka zaidi akiwa na Arsenal.
“Nadhani anastahili dau alilopewa na Asernal, Mertesacker aliliambia gazeti la Sportsmail.
‘Ni mchezaji wa aina yake na nafikiri hajafikia kiwango cha mwisho kwa sasa, ana nafasi ya kutisha zaidi”.
”Atafaa
sana. Ataifaa Asernal. Wote tunahitaji kucheza na yeye tukiwa timu
moja, nadhani mchango wake kwa klabu utakuwa mkubwa sana”.
Beki kisiki: Per Mertersacker amesema Arsene Wenger amepata jembe la ukweli, Mesut Ozil
Usajili wa nguvu: Nyota raia wa Ujerumani, Mesut Ozil alijunga na Arsenal akitokea Real Madrid
Dume la nguvu: Mesut Ozil alikamilisha uhamisho wake kujiunga na Arsenal siku ya mwisho ya usajili
Ujerumani:
Per Mertesacker alihudhuria mkutana na waandishi wa habari wakati wa
mechi ya kuwania kufuzu fainali ya kombe la dunia dhidi ya visiwa vya
Faroe Islands
0 comments:
Post a Comment