Monday, September 16, 2013

Kocha wa Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bora, Ernie Brandts akisalimiana na THEOPISTA JEROME, Msaidizi wa meneja wa kiwanda cha  TBLMbeya DIDA AKITAZAMA MTAMBO WA KUPIKA BIAMlinda mlango wa Yanga, Deogratius Munish “Dida” akitazama mtambo wa kupikia bia MFANYAKAZI WA TBL MBEYA, ROBERT ANDREW akiwaelekeza wachezajiMfanyakazi wa TBL Mbeya, ROBERT ANDREW akiwaelekeza wachezaji
Na Ibrahim Kyaruzi, Mbeya
WACHEZAJI wa Yanga inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager leo wamefanya ziara kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kilichopo maeneo Iyunga. Katika ziara hiyo mjini Mbeya na kujionea mambo mbalimbali, ikiwemo mfumo mzima wa utayarishwaji bia hadi kupakiwa tayari kuingia sokoni.
Walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali wakati wanatembezwa kwenye kiwanda hicho na wafanyakazi wa TBL Mbeya na kwa ujumla ilikuwa ziara yenye maufaa kwao.
Wafanyakazi wa TBL Mbeya walifurahi kukutana na wachezaji wa Yanga na wengine walichukua fursa hiyo kupiga nao picha za ukumbusho.
Kwa upande wake, Meneja Matukio wa Kampuni hiyo mjini hapa, Godfrey Mwangungula alisema kwamba kiwanda cha TBL Mbeya kinashikilia tuzo ya kiwanda bora cha bia Afrika kwa miaka mitatu mfululizo hivyo ni faraja kwao kutembelewa na mabingwa wa Tanzania.
Yanga kwa pamoja na wapinzani wao wa jadi, Simba SC na timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars- wote wanadhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager inayozalishwa na TBL.
Yanga iko hapa Mbeya tangu Jumatano kwa ajili ya mechi zake mbili za Ligi Kuu dhidi ya timu za hapa. Mchezo wa kwanza ilicheza Jumamosi Uwanja wa Sokoine na kulazimishwa sare ya 1-1 na Mbeya City wakati keshokutwa itahitimisha mechi zake za hapa kwa kumenyana na Prisons kwenye Uwanja huo huo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video