Friday, September 27, 2013

Miss-Universe-Tanzania-2012 
Na Mwandishi wetu
Nani atatwaa taji laMiss Universe Tanzania, jibu la swali hilo litajulikana leo (Ijumaa) wakati warembo 15 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania watakapochuana kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini kuanzia saa moja kamilli usiku.
Warembo hao mbali ya kuwania taji la Miss Universe Tanzania ambalo kwa sasa linashikiliwa na Winfrida Dominique, pia watawania taji la Miss Earth Tanzania na kupata tiketi ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa.
Warembo hao kwa nyakati tofauti waliokuwa wakitambiana huku kila mmoja akisema atatwaa taji hilo na kuiwakilisha nchi katika mashindano ya dunia yaliyopangwa kufanyika  Novemba 9 jijini Moscow, Russia.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications inayoandaa mashindano hayo, Maria Sarungi alisema kuwa kila kitu kimekamilika na warembo wamepania kufanya makubwa jukwaani . Maria alisema kuwa warembo wote wana ari ya juu na kila mmoja akiwa na shauku ya kutwaa taji hilo.
“Kwa upande wetu, kila kitu kipo tayari, warembo wamejiandaa vilivyo na tumeandaa shoo bora na fupi, hivyo mashabiki wa masuala ya urembo wanatakiwa kufika mapema ili kuona nani anatwaa taji na kupata tiketi ya kuiwakilisha nchi kimataifa,” alisema Maria.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video