Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
NAHODHA wa Manchester City, Vincent Kompany yuko hatarini kuukosa mchezo wa watani wa jadi wa jiji la Manchester “Manchester derby” mwishoni mwa mwezi huu kati ya Mnchester City dhidi ya Manchester United baada ya taarifa kuonesha kuwa nyota huyo atakaa nje ya uwanja mpaka mwezi wa 10 kutokana na majeraha ya kinena.
Kompany aliumia katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu soka nchini England dhidi ya Newcastle United `paka weusi` katika dimba la Etihad.
Awali Kompanyalitarajiwa kureja uwanjani katika mechi ya United septemba 22, lakini kocha wake Manuel Pellegrini ameachwa hoi na taarifa za nyota huyo kutorejea katika kipute hicho.
Janga kubwa: Vincent Kompany anaweza kukaa nje ya uwanja mpaka mwezi oktoba na ataikosa mechi ya watani wa jadi
Shabiki: Kompany alikuwa shabiki katika mchezo wa timu yake ya taifa ya Ubelgiji dhidi ya Scotland 2-0 katika dimba la Hampden Park jana ijumaa na timu yake kushinda 2-0
0 comments:
Post a Comment