Monday, September 16, 2013

Sehemu ya watu waliojitokeza katika kambi ya matibabu ya bure katika kijiji cha Kerege Bagamoyo. Kambi hiyo ni ya tatu kufanyika  na zaidi ya watu 600 walijitokeza kupatiwa huduma mbalimbali ikiwemo kupatiwa miwani, vyandarua na dawa bure. Pic 05 
Daktari Jaynika Solanki akimpima shinikizo la damu Amina Salum (6) mkazi wa kijiji ya Kerege Bagamoyo katika kambi ya matibabu ya bure iliyofanyika jana kijiji Cha Kerege Bagamoyo Pic 06 
Rais wa Klabu ya Rotary Dar es salaam Bi Nadine Atallah akizungumza na waandishi wa habari jana katika kambi ya matibabu ya bure iliyoratibiwa na Rotary Club Daressalaam
……………..
ROTARY CLUB OYSTERBAY LOGO1
Klabu ya Rotary Dar es Salaam Oysterbay kupitia miradi ya huduma iliyotengenezwa kuimarisha miundombinu ya usafi na afya katika jamii, inafanya shughuli mbili ambazo zinatarajiwa kuboresha maisha ya wakazi wa wilaya ya Bagamayo kwa miaka ijayo. 
Shughuli ya kwanza kati ya hizo ni kukabidhi mradi kamili wa miundo mbinu ya maji taka uliogharimu milioni 28 fedha za kitanzania hapo tarehe 14 Septemba 2013 na ya pili, tarehe 15 Septemba 2013 kutakuwa na kambi ya matibabu ambapo wataalamu kadhaa wa afya wa kujitolea watawahudumia zaidi ya wakazi 700 wa Bagamoyo kwa matatizo mbalimbali ya kiafya na magonjwa.
MAKABIDHIANO YA MRADI WA USAFI
Klabu ya Rotary ya Oysterbay imekarabati miundo mbinu ya maji taka katika shule mbili za msingi Kerege na Mapinga, kwa kujenga vyoo vipya, kuunganisha umeme, kuweka mabomba ya maji, mfumo wa usafishaji maji unaoweza kuzalisha maji safi ya kunywa, n.k, vyenye jumla ya shilingi milioni 28 fedha za kitanzania.
Makabidhiano hayo yatafanyika katika kila shule na yanategemewa kuhudhuriwa na wanafunzi, walimu, maafisa wa shule, viongozi wa mitaa na wana klabu wa Rotary.
KAMBI YA MATIBABU
Kambi ya matibabu, ambayo kwa sasa imekuwa ni tukio la kila mwaka, ipo katika mwaka wake wa tatu na itafanyika Jumapili, Septemba 15. Wanataaluma na wataalam wa tiba watawapima takribani watu 700 wenye magonjwa mbalimbali yakiwemo malaria, upungufu wa damu, kisukari na shinikizo la damu na kwa mara ya kwanza, watapima kansa ya kizazi. Pia upimaji wa hiari wa virusi vya UKIMWI utakuwepo. Kambi ya mwaka huu itajikita katika kuzuia malaria, elimu, matibabu, naiwapo akiba itaruhusu, vyandarua vya bure vitatolewa kwa washiriki wa kambi. Kila mgonjwa atapatiwa taarifa za jumla za kiafya zinazoonesha magonjwa mengine yaliyozoeleka na sababu hatarishi. Ushauri nasaha utatolewa juu ya mienendo ya maisha kama vile lishe na umuhimu wa mazoezi. 
Zaidi ya madaktari 50 na wafanyakazi wasaidiziwatakuwa wakisaidia katika usajili, upimaji na ugawaji wa vyandarua. Vipimo vyote, ushauri nasaha, na ushauri wa kitabibu utatolewa kwa wagonjwa bure. Rufaa kwenda hospitali zitatolewa penye uhitaji wa kufanya hivyo. 
“Lengo la kambi ni kuleta huduma za msingi za afya zilizobora kwa watu ambao vinginevyo wasingeweza kuzipata,” alisema Vikash Shah,mkurugenzi wa kamati ya miradi ya huduma ya Klabu ya Rotary Dares Salaam Oysterbay.
Mradi huu usingewezekana bila ya fedha zilizokusanywa katika kampeni ya uchangishaji fedha ya Rotary Dar Marathon, klabu ya Rotary ya Vancouver,  na Rotary International zilizofanyika kwa njia ya Ruzuku Linganishi.
“Tunafurahana kujivunia kwamba kupitia jitihada za pamoja kati ya jamii, wana Rotary wa kitaifa na kimataifa, taasisi zisizo za kiserikali, jamii ya kitabibu na makampuni ya kibiashara; tumeweza kuandaa kambi hii ya matibabu kwa mara ya tatu,” alisema Nadine Atallah, Raisi wa klabu ya Rotary Dar es Salaam Oysterbay 2013-2014. Aliongeza kuwa,“mradi huu utafanyika pasipo na vikwazo na tutaihudumia jamii zaidi na tunatazamia mafanikio kupitia ushirikiano kwa miaka ijayo.”
Kambi inaratibiwa kwa ushirikiano wa Shree Hindu Mandal Hospital kwa kusaidiwa na KidzCare Tanzania, Sanitas Medical Centre, Tanzania Health Promotions Support, The Tanzania Diabetes Association, ICAP,Sayona, Trinity Promotions Ltd, Vesper Security, Knight Support, Aga Khan Hospital, Aga Khan University, Jamana Printers, Supplies Stores & Jai Ambe Balvi Padmavati na ELIMIKA.
Mbali na hao, “Seattle4 Rotary Clubs” kutoka Seattle, Washington, USA ambao wamechangia kwa kiasi kikubwa mradi wa upimaji wa malaria na vifaa vitakavyokuwepo siku hiyo, pia watahudhuria.
HISTORIA 
Kambi ya kwanza ya matibabu ya bure ilifanywa na klabu mwaka 2011 katika eneo la Chanika na zaidi ya watu 600 walipimwa malaria, virusi vya UKIMWI, kisukari, magonjwa ya masikio,puana Koo (ENT), macho na dalili hatarishi za magonjwa sugu. Dawa na miwani za bure zilitolewa kwa wale waliopimwa na kugundulika na matatizo ya kiafya na matatizo ya kuona.Mwaka 2012 tulihudumia zaidi ya watu 700. Mwaka huu pia inategemewa idadi sawa ya watu watasajiliwa kwa utaratibu wa kwanza kuja wa kwanza kudumiwa.
About Rotary
Rotary Internatinal ni Shirika la kwanza duniani la klabu za huduma lenye wananchama zaidi ya milion 1.2 katika vilabu 33,000 duniani kote. Wanachama wa Rotary ni viongozi wa biashara wanaofanya kazi kitaifa, kikanda na kimataifa kwajili ya kupambana na njaa, kuboresha afya na usafi wa miundombinu ya majitaka, kutoa elimu, kuhamasisha amani na kutokomeza polio. Kaulimbiu yetu ni “Huduma zaidi ya Binafsi”.
Klabu ya Rotary Dar es Salaam Oysterbay inawakaribisha wanachama wapya. Kwa maelezo zaidi kuhusu klabu, wanachama wake, na kazi za kijamii Tanzania nzima, tembelea www.rotarydar.com.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video