Na Baraka Mpenja, Mbeya
KUFUATIA
maneno ya hapa na pale kuibuka na kuushutumu uongozi wa Simba kuwa
wamechelewa kumtibu goti winga wake, Kiggi Makassi na kuonekana kama
hawajali wanandinga wake, hatimaye ukimya wavunjwa na sasa safari
imeiva, huku maandalizi yote yakikamilika.
Kwa
taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa, Kiggi
anaondoka leo kuelekea nchini India kwa matibabu ya goti lake.
Afisa
habari wa klabu ya Simba, Ezekiel Kamwaga kupitia ukurasa wake katika
mtandao wa kijamii wa Facebook, amesema Makassi anaondoka leo saa 10:45
jioni kwa ndege.
Kamwaga
amesema kila kitu kipo sawa na kwa sasa Makassi ndio anaelekea uwanja
wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam tayari
kwa safari hiyo.
Nyota
huyo aliyesainishwaa na Simba akitokea kwa wapinzani wao wa jadi, klabu
ya Yanga, anaendea kufanyiwa upasuaji wa goti ambalo limemuweka nje ya
uwanja kwa muda mrefu.
“Tumwombee
Kiggi kwani oparesheni ya goti ni ngumu sana, hivyo Watanzania kwa
ujumla, mashabiki na wanachama wa Simba waombe dua njema kwa kijana
wao”. Alisema Kamwaga.
Siku
za nyuma Kiggi aliwahi kutajwa kwenda kwa mganga wa jadi kwenda kutibu
goti lake kwa madai kuwa viongozi wa Simba bado hawajaamua kumpeleka
katika matibabu bora, lakini uongozi wa Simba kupitia kwa mwenyekiti
wake, Alhaj Ismail Aden Rage ulisema kuwa unajiandaa kumpeleka India na
kusema kuwa mchezaji hapelekwi huko kama anapelekwa sokoni.
“Unapompeleka
mchezaji India lazima uwa na miadi na madaktari wa huko, huwezi
kumpeleka kama wampeleka sokoni bwana.. lazima mjue, Simba tunajiandaa
na kuwasiliana na wenzetu wa India, itafika wakati lazima ataondoka”.
Alikaririwa Rage.
Sasa yametimia na safari ya nyota huyo imeiva na leo hii anakwea pipa.
Dawati la michezo mtandao wa MATUKIO DUNAINI
linamtakia kila la heri Kiggi Makassi katika safari yake ya India na
Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema amsaidie katika upasuaji wake ili arejee
uwanjani na mashabiki waendele kupata raha kutoka kwake.
0 comments:
Post a Comment