Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
SASA amedhihirisha kuwa ni mchezaji ghali zaidi katika sayari hii ya tatu yaani Dunia.
Jana Gareth Bale akiwa anapasha misuli yake moto wakati wa mapumziko, alivamiwa na mashabiki wawili wa soka ambao wametafsiriwa kama waliingia kufurahia nafasi ya kumuona nyota huyo wa dunia.
Nyota huyo wa Real Madrid mwenye thamani ya pauni milioni 86 alionekana kushangazwa baada ya mashabiki kuingia uwanjani wakati wa mapumziko na yeye akiwa anapasha pasha , lakini lengo la mashabiki hao lilikuwa kufurahi naye huko Macedonia.
Karibu sana: Mashabiki wawili waliingia kumzonga Gareth Bale wakati akipasha misuli moto kipindi cha mapumziko
Winga huyo wa Wales alikuwa akifanya mazoezi ya kuweka sawa misuli yake pamoja na mchezaji mwenzake wa akiba, Adam Matthews wakati alipovamiwa na mashabiki hao wawili.
Kiungo wa Celtic Matthews alimsaidia Bale ili kulinda usalama wake kabla ya wana usalama kufika , na Bale alikuwa anacheka tu kutokana na tukio lile.
Wawili wameingia: wavamizi wa uwanja wakumzonga Gareth Bale wakati wa mapumziko
Anasaidiwa: TV ilionesha mchezaji mwenzake Adam Matthews akimsaidia Bale
Bale amesaidiwa: wana usalama wakiwadhibiti wahalifu hao
Lakini hiyo ni kengele ya kumkumbusha Bale mwenye miaka 24 kuyazoea maisha ya `usupa staa` baada ya kuvunja rekodi ya usajili ya dunia akitoka klabu ya Spurs ya kaskazini mwa London, nchini England.
Bale alikuwa mchezaji wa akiba katika mchezo wa jana wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia huko Skopje ambako walipoteza mchezo kwa mabao mawili 2-1.
Vijana wa soka: Bale na Matthews wakipasha moto misuli kipindi cha mapumziko
Wamekalia benchi
0 comments:
Post a Comment