Friday, September 27, 2013


Na Baraka Mpenja , Mbeya
KIUNGO wa zamani wa klabu ya Simba na Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa stars aliyetoroka kambini mwezi julai mwaka huu wakati Stars ikijiandaa na mechi ya kuwania kufuzu kombe la Dunia dhidi ya Uganda `The Cranes` katika uwanja wa Namboole Kampala, Mwinyi Kazimoto Mwitula  ametuma salamu za shukurani kwa mashabiki wa Simba, viongozi na watanzania wote waliokuwa wanamuunga mkono.
Ujumbe ambao Kazimoto ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook maarufu kwa jina la FB amesomeka kama ifuatavyo;
“Najua sikupata muda wa kuwashukuru watanzania wote waliokua wananiunga mkono kwa support yao siku zote kwanza,, haswa haswa wapenzi wa simba,viongozi,wanachama kwa kunivumilia kwa mabaya na mazuri yote,,,nawatakia simba mafanikio mema kwenye ligi……pamoja sana…”.
Jembe la kazi!: Kazimoto Alitoroka kambi ya timu ya Taifa, Taifa Stars akiwa jijini Mwanza kujiandaa na mchezo dhidi ya Uganda, lakini aliomba radhi na yakaisha. Sasa anag`ara huko Qatar.

Ikumbukwe kuwa Kitendo alichokifanya nyota huyu kutoroka katika kambi ya Taifa kilitafsiriwa kuwa ni kukosa uzalendo kwani Stars ilikuwa inakabiliwa na mchezo mgumu zaidi.
Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen alisikitishwa sana na kitendo alichofanyiwa na kiungo wake tegemeo katika kikosi chake, lakini baadaye zilitoka taarifa kuwa ametimkia Qatar kwenda kucheza soka la kulipwa na kim kubariki mafanikio ya nyota wake.
MWINYI 
Mkali wa kumiliki gozi na kupiga pasi za uhakika: Mwinyi kazimoto enza zake akiwa Simba kuonesha maujuzi ya hali ya juu

Baadaye Kazimoto alijitokeza na kuandika barua ya wazi akiwaomba radhi watanzania, shirikisho la soka Tanzania, TFF, Uongozi wa Simba kwa kitendo alichofanya.
Kazimoto alieleza kuwa siku zote alikuwa ana ndoto ya kucheza soka la kulipwa, hivyo baada ya kupata timu Qatar alishawishika kutoroka kwani nafasi ilikuwa adimu na ya haraka kwake. Lakini baadaye kuna taarifa zilitoka kuwa alitoroka kwasababu kuna baadhi ya watu walimkera.
Kazimoto ambaye kabla ya kujiunga na Simba, alikuwa anakipiga kwa maafande wa Jeshi la kujenga Taifa, JKT Ruvu kutoka mwaka 2007-2011 na akajiunga na wekundu wa Msimbazi Simba mwaka 2011 na kuwa kiungo tegemeo mpaka anaondoka mwaka katikati ya mwaka huu.
Kijana huyo anawavutia wapenzi wengi wa soka kwa uwezo wake wa kupiga mashuti na kufunga mabao ya mbali, lakini pia kumiliki mpira na kupiga pasi za uhakika.
Kwa sasa nyota huyo mzaliwa wa mwaka 1988 mjini Dodoma anakipiga huko nchini Qatar katika klabu ya Al Markhiya.
0017 
Wakati huo huo, nahodha wa mabingwa watetezo wa ligi kuu soka Tanzania bara, Nadir Haroub `Canavaro` amefurahishwa na kitendo cha uongozi wa timu yake chini ya mwenyekiti Yusuf Manji kumaliza sakata la Mrisho Ngassa kwa kukubali kulipa deni la milioni 45 kwa klabu ya Simba SC na kutoa kauli kuwa sasa kesho ndio wanaanza ligi dhidi ya Ruvu Shooting.
Canavaro ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook ambao mara nyingi huwa anautumia kutoa kauli tofauti kwa mashabiki wake kuwa;
“Habari’  Mwenyekiti kayamaliza..kesho tunaanza kazi…. #yangadaimambele
Ujumbe huu hauko moja kwa moja, lakini kutokana na sakata la Ngassa kuwa habari ya mjini kwa sasa na uongozi kukubali kulipa deni lake na kusema kuwa nyota huyo atacheza kesho, inatosha kujiridhisha kuwa Canavaro anamaanisha urejeo wa nyota huyo baada ya kifungo cha mechi 6.
Wakati hayo yakijiri, naye kocha msaidizi wa Yanga, Fred Ferlix Minziro amekaririrwa na vyombo vya habari akisema kuwa kesho Ngassa atakuwa miongoni mwa wachezaji 11 watakaoanza katika kikosi cha kocha Ernie Brandts dhidi ya Ruvu Shooting katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video