Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
KOCHA
wa timu ya Taifa ya England, maarufu kwa jina la `Simba Watatu` Roy
Hodgson ameielezea mechi ya kesho dhidi ya Ukraine mjini Kiev kuwania
kufuzu fainali za kombe la Dunia mwakani nchini Brazil kuwa ni kama
mechi ya fainali ya kombe hilo kubwa duniani.
Mataifa
hayo mawili yanatofautiana kwa pointi moja tu katika kundi lao la H na
yamebakiwa na mechi tatu, huku kila taifa likihitaji ushindi na kufuzu
kwenda Brazil.
Hata
hivyo Hodgson amethibitisha kuwa kiungo mkongwe, Frank Lampard
atafikisha mechi ya 100 akiichezea timu yake ya Taifa katika uwanja
Olympic mjini Kiev hapo jesho usiku na lengo lake ni kubadili timu
iliyoanza dhidi ya Moldova ijumaa usiku.
Mpaka Brazil: Hodgson na Gerrard wakiongelea mchezo mkali wa kesho usiku dhidi ya Ukraine mjini Kiev
Hodgson
alisema: “Ni kama mechi ya fainali na tumeupa heshima hiyo, lakini
tunatakiwa kucheza kadri iwezekavyo kupata ushindi. Tunatakiwa kupigana.
Wachezaji wanajua tunachotaka na wanajiamini sana”.
Lampard
atacheza sambamba na wakali wenzake waliofikisha mechi 100 wakiichezea
timu yao ya Taifa, nahodha Steven Gerrard na mlinzi Ashley Cole.
Wanakula
bata kabla ya kazi kesho: Wachezaji wa timu ya Taifa ya England
wakitembea tembea mjini Kiev leo mchana mjini Kiev kabla ya kibarua cha
kesho dhidi ya Ukraine
Tabasamu la nguvu: Lampard kesho atafikisha mechi ya 100 akiichezea timu yake ya Taifa ya England
Kazi nzuri: England walifurahia ushindi dhidi ya Moldova, lakini watawakosa wafungaji wao wawili wa mabao mawili
0 comments:
Post a Comment