Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
BAADA
ya mishemishe zote, hatimaye, Gareth Bale ataitumikia kwa mara ya
kwanza klabu yake ya Real Madrid mwishoni mwa wiki hii-lakini anaweza
akatumika nafasi ya beki wa kushoto?
Mchezaji huyo mwenye thamani kubwa zaidi duniani atakuwa beki pekee wa kushoto katika kikosi cha
Carlo Ancelotti baada ya mabeki wote wa pembeni Marcelo na Fabio
Coentrao kupata majeruhi katika mechi zao za kimataifa na timu zao za
Taifa.
Mbrazil
Marcelo aliumia mguu wakati wa mechi ya kirafiki baina ya timu ya
Taifa ya Brazil dhidi ya Australia wikiendi iliyopita ambapo vijana hao
wa Samba walishinda mabao 6-0 na alikosa mechi ya leo mapema dhidi ya
Ureno, mechi ambayo Brazil wameshinda mabao 3-1.
Jembe la ukweli: Gareth Bale alitokea benchi katika mechi ya Timu yake ya Taifa ya Wales jumanne usiku
Je, ataweza kufurukuta kwa mara ya kwanza?
Janga: Fabio Coentrao aliumia katika mchezo wa kirafiki baina ya Brazil na Ureno
Wasiwasi:
Marcelo (kushoto) ameumia pia na hii ina maanisha Bale anaweza kucheza
mechi ya kwanza akiwa Real madrid nafasi ya beki wa kushoto
Mtu
muhimu: Bale alikamilisha uhamisho uliovunja rekodi ya dunia wa pauni
milioni 86 kutoka Spurs ya England kujiunga na Real Madrid wiki
iliyopita
0 comments:
Post a Comment