Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
KLABU
ya Real Madrid inatarajia kusajili mshambuliaji mpya katika dirisha
dogo la usajili januari mwakani ambapo amewaweka katika rada zake, nyota
wa Liverpool, Luis Suarez na mashine ya Monaco, Radamel Falcao , na
hii ni kulingana na gazeti la Hispania la Marca.
Majira
ya usajili ya kiangazi, Miamba hiyo ya soka la Hispania aliwauza
washambuliaji wake, Gonzalo Higuain na Jose Callejon kwenda klabu ya
Napoli na kuwaacha wawili tu, Karim Benzema na kinda Alvaro Morata
wakiwa ni washambuliaji wa katikati.
Japokuwa
Cristiano Ronaldo anaweza kucheza akiwa mshambuliaji wa kati, lakini
kocha Carlo Ancelotti anataka kutumia pesa aliyonufaika katika mauzo ya
Mesut Ozil kwenda Arsenal kununua mshambuliaji mpya.
Kwenye rada: Gazeti la Marca limeeleza kuwa Real Madrid wanamuwania Suarez au Falcao katika dirisha dogo la usajili
Hakuwa na furaha: Suarez alitumaini kuhama Liverpool wakati wa majira ya kiangazi
Jembe jipya: Falcao alijiunga na Monaco mwezi wa tano mwaka huu, lakini tayari anahusishwa kujiunga na Real Madrid
Dau kubwa; Florentino Perez akiwa na Gareth Bale baada ya kumsainisha kwa dau lililovunja rekodi ya Dunia
Presha kubwa: Benzema ndiye mshambuliaji mkongwe pekee aliyesalia Real Madrid
0 comments:
Post a Comment