Wednesday, September 25, 2013

BAADA ya kuwatafuna `Kwalalumpa Malysia`, klabu ya Yanga ya Dar es salaam mabao 3-2 jumapili ya wiki iliyopita, matajiri wa kuoka mikate, wana Lambalamba, Azam FC wanaendelea kujifua vilivyo kuwakabili maaskari wa jeshi la Magereza, Tanzania Prisons `Wajelajela` mwishoni mwa wiki hii katika dimba la kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Dar es salaam `Jiji la maji chumvi`, Afisa habari wa klabu hiyo, Jafar  Idd Maganga amesema wanatambua ugumu na ukongwe wa Prisons katika michuano ya ligi kuu, hivyo wanajipanga kuhakikisha wanapambana kufa na kupona ili kupata pointi tatu muhimu ugenini.
“Sisi tunaendelea vizuri na mazoezi, lengo letu ni kupata pointi tatu muhimu. Tunajua itakuwa mechi ngumu sana kwetu kwani Prisons wana uzoefu mkubwa. Panapo majaaliwa tunaondoka kesho kuelekea Mbeya ili kuwaruhusu wachezaji wetu kuzoea hali ya hewa ya jiji hilo ambayo ni ni tofauti na Dar es salaam”. Alisema Jafar.
Mshambuliaji hatari wa Azam fc, John Raphael Bocco `Adebayor naye atakuwepo jijini Mbeya jumapili
Jafar alifafanua kuwa wachezaji wote wako salama, wana morali kubwa kuelekea mchezo huo ambao wanauheshimu sana kutokana na ugumu wa wajelajela wanapokuwa katika dimba lao la nyumbani.
“Msimu wa mwaka jana tulikutana na Prisons kwao na kuambulia pointi moja, kiukweli ni wapiganaji sana wakiwa kwao, lakini sisi Azam fc kila mchezo ni fainali kwetu, tuko tayari kupambana”. Alijigamba Jafar.
TFF Tanzania Prisons 
Kikosi cha Tanzania Prisons msimu uliopita ,(Picha na Makataba)
Wakati huo huo, Maafande wa Tanzania Prisons wapo chimbo kujiandaa na kipute hicho cha kukata na shoka kwa lengo la kupata ushindi wa kwanza baada ya kufungwa mechi mbili ugenini, kutoka sare moja ugenini na mbili nyumbani.
Katibu mkuu wa Prisons, Inspecta Sadick Jumbe ametamba kuwaadibisha wana lambalamba kutokana na kikosi chao chini ya kocha mkuu Jumanne Chale kuimarika na kufuta makosa ya mechi za awali.
“Utakuwa mchezo mgumu kwetu, Azam watachagizwa na ushindi walioupata dhidi ya Yanga, tuko nyumbani na tutatumia vizuri nafasi hii kupata matokeo ya ushindi na kuwafurahisha mashabiki wetu”. Alisema Jumbe.
Aidha katibu huyo amewaomba mashabiki wa kandanda jijini hapa kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kuwapa hamasa kubwa wanandinga wao.
Mbali na mchezo huo wa jumapili (Septemba 29), kutakuwa na michezo mingine ya ligi kuu ambapo Jkt Ruvu watakuwa dimba la Taifa jijini Dar es salaam kuvaana na wekundu wa Msimbazi Simba.
Vibonde wa ligi hiyo, wauza mitumba wa Ilala, Ashanti United watakuwa Azam Complex mbande Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam kukwaruzana na wakata miwa wa mashamba ya Manungu Turiania mkoani Morogoro, klabu ya Mtibwa Sugar.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video