Tuesday, September 10, 2013

00000000000nchimbi na chagonja 4
Na Buberwa Jackob
Kwanini Vibali vyote vya kuishi wageni visifutwe na kusajiliwa upya?.  Msako lazima uwe na kasi kubwa tena uanzie mji mikubwa kama Dar, Arusha…
Kuanzia mwezi julai 2013 kiongozi mkuu wa nchi yetu rais Dk.Jakaya Kikwete katoa agizo kuwa raia wote wa kigeni ambao ni wahamiaji haramu wamepewa siku 14, kuondoka au kujisalimisha katika vyombo vya dola.
Agizo hili la rais lina lengo zuri tu kwa watanzania na usalama wa watanzania, lakini utekelezwaji wake umekuwa hauna kasi, kwani idadi ya wahamiaji haramu walio jisalimisha ni ndogo kulingana na waliopo nchini, na kati ya hao waliojisalimisha ni wahamiaji waliopo nje ya miji mkubwa sio katika miji mikubwa kama Dar ,Arusha nakwingineko !
Cha kushangaza kwamba kuna baadhi ya wahamiaji haramu au halali wanakiuka kwa namna moja au nyingine sababu zinazowafanya kuwepo nchini Tanzania. mfano raia wa kigeni aliyekuja nchini kwa kufanya kazi fulani na akapewa kibali kwa ajili hiyo anakiuka kwa taratibu za uhamiaji na kuanza kuwa mfanyi biashara ya baa au dangulo fulani! au pengine kujiingiza katika biashara ambayo mzawa anaweza kuifanya, na huku vyombo vya usalama vikimwangalia !
Hivi kuna uhalali wa kisheria Raia wa kigeni asiye na hata asili ya Tanzania kumiliki nyumba au Ardhi ?
Watanzania wengi wamekuwa wakilalamika juu ya ongezeko la raia wa kigeni hususan raia wa nchi za ulaya, Asia na nchi za kiarabu kumiliki au kununua nyumba na ardhi nchini , mfano wachina wanamiliki majumba au ardhi,  huenda  wakawa wanakiuka sheria fulani za nchi,na watanzania wanao wauzia nyumba wageni hao nao pia wanajisaliti au kuisaliti nchi.
Ukiwikaji wa sheria za ajira ! mchina anapofanya kazi ya kuuza duka na mitumba au kubeba zege !  Mzungu anapokuja kutalii na baadaye  kupata ajira ya muhudumu wa hotel ! hili nalo neno?
Bendi za muziki zinapo ajiri wanenguaji kutoka nje ya nchi!
Ndio maana watanzania walio wengi wanaona kuwa ipo haja kwa serikali kuvifuta vibali vyote vya wageni na kuanza zoezi la kuvitoa upya na kuvihakiki kwa kupitia Wizara ya mambo ya ndani.
Kama Rais JK kashatoa agizo tangu mwezi julai mbona utekelezaji wake una mwendo wa pole ? wakati kiongozi mkuu wa nchi, ambaye ndiye amiri jeshi mkuu kishaagiza siku 14 tu kila muhamiaji haramu aondoke sasa kwanini  msako usianze katika kutekeleza agizo la mkuu wa nchi?.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Mbariki Rais JK

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video