Wednesday, August 7, 2013


Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Dar Young Africnas wametamba kuwabamiza wapinzania wao Azam fc  “wana lambalamba” katika mchezo wa ngao ya hisani agosti 17 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam,  kuashiria kufunguliwa pazia la ligi kuu msimu wa 2013/2014.
Akizungumza na Mtandao wa FULLSHANGWE, Afisa habari wa Yanga, Baraka Kizuguto amesema kikosi chao kinaendelea vizuri na mazoezi kujiandaa na mchezo huo muhimu kwao na wanajiandaa kushinda kutokana na klabu hiyo kusheheni wachezaji nyota wenye kiwango cha juu.
“Yanga ina kikosi kizuri mno kwa sasa, hatuna wasiwasi kabisa, sisi tunaendelea na mazoezi ya kujiandaa kuwakabili wapinzani wetu katika mchezo huo wa Ngao ya jamii”. Alisema Kizuguto.
28Kuzuguto alisema wanatambua ugumu wa mechi hiyo kwani wapinzani wao nao wana timu nzuri na wanafanya maandalizi mazuri nje ya nchi.
“Azam fc ni wazuri, itakuwa mechi nzuri sana, lakini sisi Yanga tunajiandaa kama kawaida yetu kutoa dozi, lazima tuwafunge wapinzani wetu na kutwaa kombe la ngao ya hisani ili kuendelea kuwajenga wachezaji kisaikolojia pamoja na mashabiki wetu kuelekea kutetea ubingwa wetu wa ligi kuu soka Tanzania bara”. Alisema Kizuguto.
IMG_2117Wakati Yanga wakijigamba kufanya hivyo, nao Azam fc kupitia kwa meneja wao, Jemedari Said aliyekaririwa na vyombo vya habari vya hapa Tanzania akiwa nchini Afrika kusini alisema kikosi chao kinaendelea vizuri na mazoezi nchini humo, huku wachezaji wakipata changamoto nzuri kutoka kwa klabu za huko ambazo ni bora zaidi ya klabu za ukanda wa Afrika mashariki na kati.
Said alisema walianza kwa kufungwa mabao 3-0 na Kaizer Chief inayoshiriki ligi kuu nchini Afrika kusini, lakini kwa kiasi kikubwa walipata kile walichokuwa wanakihitaji, na leo hii watacheza mechi ya pili dhidi ya Mamelodi Sundwons .
Meneja huyo alisema watarejea nchini Agosti 13 kufanya maandalizi ya mwisho kujiandaa na mchezo wa ngao ya Hisani ambapo amesema watafanya vizuri na kuwafunga Yanga kutokana na maandalizi mazuri wayapatayo nchini Afrika kusini.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video