Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kocha Brendan Rodgers amesema Liverpool ina mamlaka yote ya kuamua maisha ya baadaye ya Luis Suarez na nyota huyo atafanya vizuri zaidi ya msimu uliopita baada ya kugundua kuwa haruhusiwi kundoka.
Arsenal bado wanaendelea kumshawishi Suarez ambaye msimu uliopita alikuwa mhimili wa Liverpool, na wanatarajia kuongeza dau kubwa zaidi ya pauni milioni 41 walizotuma awali na kukataliwa.
Arsene Wenger mapema jana alithibitisha kuwa ana matumaini ya kumsajili mshambuliaji huyo, lakini Rodgers alimuamuru Saurez kufanya mazoezi peke yake baada ya kurudia kauli yake ya kutaka kuondoka, ila amesema anaamnini atabakia Anfield.
‘Sisi tumetulia’ alisema Rodgers. ‘ Klabu ndiyo yenye mamlaka juu ya suala hilo. Mmiliki wa timu anajua hilo na ana akili sana, amekaa kimya na ameweka wazi na kutuunga mkono kuwa tunahitaji kuwa naye msimu ujao.
Akiendesha mkoko wake: Luis Suarez, alipigwa picha akiondoka na gari lake katika mazoezi ya jana na yupo tayari kuondoka Liverpol.
Ametulia: Brendan Rodgers anaamini Liverpool ndio wenye mamlaka juu ya hatima ya baadaye ya Luis Suarez
Haeleweki: Dili la Luis Suarez kutaka kuihama Liverpool majira haya ya kiangazi limedhibitiwa na mabosi wake
0 comments:
Post a Comment