Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kiungo Mkongwe Frank James Lampard alicheza kwa mara ya kwanza majira haya ya joto, lakini alishindwa kuhimili mikikimikiki mizito ya mshambulaiji hatari wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Dos Santos Aveiro Ronaldo kuipatia shida za uwanjani Chelsea jana.
Kabla ya mechi hiyo na Real Madrid mjini Miami, kiungo huyo mkongwe alikosa mechi zote za kujiandaa na msimu za klabu, Stamford Bridge kutokana na kuwa majeruhi.
Lakini Lampard ameimarika na kuanza kazi tayari kwa mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu dhidi ya Hull City, Agosti 18 baada ya kumaliza dakika 45 za kwanza katika Fainali ya Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness.
Katika mechi hiyo, mabao mawili ya Ronaldo na moja Marcelo, yalitosha kuwalaza Chelsea Kwa jumla ya mabao 3-1.
Bao pekee la Chelsea lilifungwa na Mbrazil, Ramires.
Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Arbeloa, Pepe, Ramos, Marcelo, Modric, Khedira, Isco, Ozil, Ronaldo na Benzema.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Terry, Cahill, Cole, Lampard, Van Ginkel, Ramires, Oscar, Hazard na Lukaku.
Kama dawa kama kawaida: Cristiano Ronaldo aliwatungua Chelsea mabao mawaili jana
Fulll bata : Nyota wa Real Madrid wakiwa pamoja kushangilia ndoo yao ya mabingwa wa kimataifa wa Guinness baada ya kuwatungua Chelsea
Ronaldo akifunga bao kwa njia adhabu
Hatuna shida: Shabiki wa Real Madrid akiwa na bango liliondikwa kuwa hawajali hata kama Mourinho ameondoka klabuni kwao
Vipi mtu wangu, utaweza presha ya pale?: Mourinho na kocha wa zamani wa Chelsea , na sasa kocha wa Madrid, Carlo Ancelotti, wakipiga stori kidogo baada ya mechi kumalizika
0 comments:
Post a Comment