Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
David Moyes ameendelea kukumbwa na wingu zito machoni kwake wakati huu wa usajili baada ya kocha wa Everton, Roberto Martinez kuibuka na kusema beki wake nguli, Leighton Baines hatajiunga na Manchester United majira haya ya kiangazi.
Moyes amekuwa akihusishwa na mbio za kutaka kumchukua beki huyo wa kushoto, lakini Martinez amesisitiza kuwa dau ka mwisho la United walilotuma mwezi juni mwaka huu la pauni milioni 12 lilikuwa la mwisho na wao hawaoni kama dau hilo linaendana na thamani ya beki huyo kisiki.
Pia mchezaji mwingine wa Erveton Marouane Fellaini amekuwa akihusishwa kujiunga na kocha wake wa zamani, Moyes katika dimba la Old Trafford, lakini kocha wa Everton amesisitiza kuwa Baines hataondoka.
Kaa hapa kijana: Martinez amesema Manchester United wameshafika dau lao la mwisho kwa Baines, hivyo wasahau kumpata
Karibu klabuni: Martinez akizungumza wakati wa chakula cha mchana jijini Liverpool jana
“Kabla hatujaenda Austria klabu moja ilikuwa na mawasiliano na sisi na kufika ofa ya mwisho; Martinez amewaambia Liverpool Echo.
‘Waliweka ofa yao na dau lao lilikuwa haliendani na thamani ya Leighton Baines”.
0 comments:
Post a Comment