Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez ametoa jipya tena baada ya kusema anataka kuendelea kuitumia klabu yake hiyo na kufuta mipango ya kuihama majira haya ya kiangazi, na taarifa hizi zimetoka nyumbani kwao Uruguay.
Suarez amekuwa akihusishwa na mpango wa kuondoka Anfield, lakini kwa mujibu wa taarifa za waandishi wa habari wa Uruguay zinasema heshima kubwa waliyompa na wanayoendelea kumpa mashabiki wa Liverpool imemshawishi kuendelea kufanya kazi kwa majogoo ya jiji.
Nyota huyo anayemuumiza kichwa kwa muda mrefu kocha wa Arsenal, Mzee Aserne Wenger alikuwepo leo katika mchezo wa kirafiki baina ya timu yake ya Taifa ya Uruguay dhidi ya Japan na kufunga bao la tatu kati ya 4-2 waliyoshinda mbele ya Wajapan akiwemo na nyota wa Manchester United, Shinji Kagawa.
Saurez amekuwa akimchukiza sana kocha wake Brendan Rodgers anayemtaka kubaki, lakini yeye akisema anataka kuondoka, na hali hii ilimfanya aadhibiwe kufanya mazoezi peke yake, lakini maneno haya ya leo ni faraja kubwa sana kwake.
Kwa upande wa pili, taarifa hizi ni mbaya sana kwa Wenger ambaye anahangaika sana kutaka kuinasa saini ya Suarez na tayari alishatuma ofa ya pauni milioni 41, lakini Liverpool walikataa na kuesema nyota wao hauzwi.
Mzee wa kazi: Luis Suarez, akipambana vikali wakati akiichezea timu yake ya taifa ya Uruguay dhidi ya Japan leo jumatano na amejitokeza na kusema ameamua kufuta mipango yake ya kutaka kuandoka, hivyo anabakia Liverpool kutokana na heshima anayopewa na mashabiki wa Majogoo hao wa jiji
0 comments:
Post a Comment