Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Hatimaye winga wa Liverpool, Stewart Downing yuko tayari kujiunga West Ham baada ya kukamilisha taraibu za uhamisho uliogharimu pauni milioni 6million kutoka Anfield.
Nyota huyo mwenye miaka 29, amefuzu vipimo hapo jana usiku na Liverpool wamekubali kula hasara ya pauni milioni 8, kwani walimsajili kwa pauni milioni 14 kutoka Aston Villa miaka miwili iliyopita.
Taarifa hizo zimepata nguvu zaidi baada ya mshambuliaji wa zamani wa Liverpool anayekipiga West ham Andy Carroll, ambaye ameandika katika mtandao wake wa Twita akiseama: “Usajili mkubwa kwetu leo”
Stewart Downing amesema yuko tayari kuwa na msimu mzuri zaidi baada ya kukamilisha usajili wake
Karibu swahiba: Andy Carroll ameandika katika mtandao wake wa Twita kuonesha furaha yake kwa Downing kujiunga na West Ham
Akizungumza na mtandao wa Hammers unaomilikiwa na wagonga nyundo wa London amesema : “Nimefurahi sana. Ni nafasi nzuri kwangu kuwa hapa, ni klabu kubwa na kiukweli nimefurahi kujiunga nayo”.
“Niko tayari na nipo sawa kwa mchezo wa kwanza dhidi ya Cardiff City. Nimecheza michezo michache katika klabu ya Liverpool wakati huu wa maandalizi ya ligi, hivyo hakutakuwa na tatizo lolote”.
Changamoto Mpya: Stewart Downing amejiunga na wagonga nyundo wa London, West Ham akitokea Liverpool kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 6 ambapo wamekula hasara ya pauni milioni 8, kwani wao walimsajili kwa pauni milioni 14 kutoka Aston Villa.
0 comments:
Post a Comment