Wednesday, August 14, 2013

618328941Mwenyekiti wa Yanga kama kaibuka kidedea vile
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Taarifa zilizotufikia katika dawati la michezo la Mtandao huu kutoka chanzo chetu muhimu zinasema hatimaye Mkutani ulioitishwa na Wizara ya habari, vijana, utamaduni na mchezo chini ya waziri wake, Mhe. Dkt. Fenella Mukangara kuliweka sawa suala la mgogoro wa mkataba wa mauzo ya haki za matangazo ya Television kwa ligi kuu soka Tanzania bara uliowashirikisha kamati ya ligi kuu ya TFF, klabu ya Yanga na Azam Media umemalizika hivi punde huku maamuzi kadhaa yakifikiwa baina ya pande zote.
 Kwa mujibu wa chanzo chetu, mkutano huo umeamuru kuwa baadhi vipengele vya mkataba huo kupitiwa upya kwa umakini kati ya kamati ya ligi na klabu ya Yanga, na vile ambavyo vitakuwa tofauti virekebishwe kabla ya kuanza kwa mchakato mzima wa kuwapa raha wanamichezo nchini Tanzania kutokana na kuoneshwa kwa mechi hizo.
Pia makubaliano yamefikiwa kuwa Uongozi wa Yanga utakaa kikao na Azam Media kuzungumzia mambo mbalimbali ambayo Yanga imeonekana kuwa na shaka nayo kuhusu Azam Media.
Mtandao huu unafanya jitihada za kupata taarifa zaidi kuhusiana na Mkutano huo muhimu sana kwa hatima ya soka la Tanzania, endelea  kufuatilia kupitia mtandao huu uliosheheni habari za moto moto.
Kati ya klabu 14 za ligi kuu soka Tanzania bara, Yanga pekee ndio klabu iliyokataa mkataba wa Azam Media kwa kutoa sababu mbalibali, na Mwenyekiti wake Yusuf Manji kuitisha mkutano wa dhararu wa wanachama utakaofanyika Agosti 18 kujadili suala hilo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video