Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
“Hakuna kulala, mwanaume kujituma”, David Moyes na Manchester United yake wanajiandaa kutuma ofa ya mwisho katika jaribio lao la kutaka kumchomoa Cesc Fabregas kutoka Barcelona endapo nyota huyo atajikuta hayuko katika mipango ya wazee wa Nou Camp mwanzoni mwa msimu ujao.
United wanaonekana kumshawishi Fabregas kujiunga Old Trafford, lakini mwishoni mwa wiki iliyoipita nyota huyo aliwaambia waandishi wa habari kuwa anataka kubaki katika klabu yake ya sasa.
Baada ya kutoa kauli hiyo United walisema “Tunaheshimu maamuzi ya Cesc”
Mpaka kieleweke: Manchester United wanajiandaa kutuma ofa ya mwisho kwa Cesc Fabregas licha ya yeye kusema anataka kubakia Barca
Mambo dole tu: Moyes tayari ameshatuma ofa mbili kwa kiungo wa zamani wa Arsenal na kukataliwa
Hata hivyo, Mtandao wa Sportsmail unafahamu kuwa United wanaendelea kukodoa macho kwa Fabregas na wanajiandaa kurudi tena na ofa ya mwisho itakayozidi pauni milioni 32 endapo kiungo huyo wa zamani wa Arsenal ataanza msimu ujao wa La Liga akiwa benchi.
Fabregas hatakuwepo katika mchezo wa ufunguzi wa La Liga dhidi ya Levante jumapili kutokana na kuwa majeruhi ya kifundo cha mguu aliyoyapata wakati wa michezo ya maandalizi ya ligi kuu nchini Malaysia na hatarajiwe kupata nafuu mapema.
0 comments:
Post a Comment