Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Barcelona wanaamini beki, David Luiz atawaambia Chelsea jumatatu ya wiki ijayo kuwa anataka kujiunga na mabingwa hao wa ligi ya Uhispania La Liga.
Barca walianza harakati za kutaka kumsajili Mbrazil huyo jumatano ya wiki hii lakini ilikataliwa na kocha Jose Mourinho aliwaonya kuwa wasirudi na ofa nyingine kwani hataki.
Ingawa Barcelona wanaona ugumu kumshawishi Mourinho kwa bei wanayotaka, lakini wana matumaini kuwa endapo nyota huyo atawaambia kwamba anataka kuondoka, basi ataimarisha makubaliano baina ya timu hizo mbili.
Anasubiri mchezo: Barca wanatarajia Luiz kuwapa Chelsea barua ya kutaka kuondoka siku chahce zizajo ili wamsajili
Endapo watamkosa Luiz, Daniel Agger wa Liverpool ndio mpango B, lakini nyota huyo aliteuliwa kuwa nahodha msaidizi Anfield kurithi mikoba ya Jamie Carragher aliyetandika dalagu kucheza soka.
Wiki hii Mourinho aliwamuambia kocha wa Barca Tata Martino kuwa aangalia mahala kwingine na sio kwa jembe lake Luiz
‘Ofa?, ni kupoteza muda,’ alisema Mourinho.
‘Ushauri wangu kwao ni kuangalia mchezaji wa pili katika orodha yao kwasababu wanapoteza muda. Hatutaki kuuza wachezaji wetu wazuri, hatuna muda”
Tata Martino safu yake ya ulinzi ni uchochoro vibaya sana kwa sasa, anahitaji jembe la kati
Suala la beki: Bosi wa Barca, Tata Martino anaweza kumgeukia beki wa Liverpool, Daniel Agger kama dili za Luiz litagonga mwamba
0 comments:
Post a Comment