Saturday, June 8, 2013

Yanga-Champions-300
Na Baraka Mpenja
Mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara na mabingwa watetezi wa kombe la Kagame, Dar Young Africans wanaendelea vizuri na mazoezi yake ya kujiandaa na michuano ya kombe la Kagame licha ya nyota wake muhimu kukosekana kufuatia kuwa na majukumu ya timu za taifa.
Katibu mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako ameimbia MATUKIO DUNIANI Kuwa klabu hiyo haiangalii Kagame tu bali wana mipango mingi hususani ushiriki wao katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika mwakani.
Mwalusako alisema wanajiandaa kushiriki michuano ya kimataifa, kutetea ubingwa wao msimu ujao na kombe la Kagame mwaka huu, hivyo watu wanaosema Yanga wanajiandaa na Kagame tu, wanatakiwa kukaa kimya.
“Yanga tuna mipango mingi sana, Kagame sio kitu kwetu, lakini tunajipanga sana, tunashiriki michuano mikubwa zaidi ya Kagame, tunatakiwa kufanya vizuri zaidi michuano ya kimataifa ili kujenga heshima kwa mataifa mbalimbali barani Afrika”. Alisema Mwalusako.
Katibu huyo wa wanajangwani aliongeza kuwa kwa sasa wachezaji kadhaa wa kikosi cha kwanza wapo na timu ya taifa ya Tanzania nchini Morocco, huku wale wa kimataifa wakiwa na timu zao za taifa akiwemo Haruna Niyonzima, lakini watakaporejea mambo yatazidi kunoga zaidi.
Pia Mwalusako aliongeza kuwa baada ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu msimu uliopita, wanaandaa ziara ya mikoani kwa lengo la kuongea na wanachama wao pamoja na kuwaonesha kombe lao.
“Tutapita mikoa mbalimbali hapa nchini, lengo ni kuwaonesha ubingwa wetu na kuongea nao kwa lengo la kujenga umoja na mshikamano wa klabu yetu, tunaandaa ziara hiyo na mambo yanakwenda vizuri”. Alisema Mwalusako.
Yanga wataiwakilisha Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika msimu ujao baada ya kuwapokonya watani wao wa jadi ubingwa , wekundu wa Msimbazi Simba waliomaliza katika nafasi ya tatu kigumu sana, baada ya kukabwa koo na Kagera Sugar kwa muda.
Michauno ya mwaka huu Simba waliiwakilisha Tanzania na kutolewa hatua ya awali baada ya kufungwa na Libolo ya Angola bao 1-0 uwanja wa taifa Dar es salaam, na  mechi ya marudiano walipigwa bao 4-0 nchini Angalo.
Mwaka ujao ni zamu ya Yanga kucheza ngoma hiyo nzito barani Afrika.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video