Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akionyesha msisitizo alipokuwa
akiwasilisha mada kuhusu fikra za kibunifu kwa ajili ya kuinua uchumi
kwa wanafunzi wa elimu ya juu leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akitoa mfano wa mabadiliko ya
kiteknolojia kwa kutumia mfano wa Simu za mkononi leo jijini Dar es
Salaam
Baadhi
ya washiriki wa mjadala kuhusu fikra za kibunifu kwa ajili ya kuinua
uchumi kwa wanafunzi wa elimu ya juu wakifuatilia mada leo jijini Dar
es Salaam.
Mwakilishi
kutoka Kampuni ya Breco inayojishughulisha na miradi ya kukamua Alizeti
Kibaigwa Dodoma Bi Tatu Shamte akielezea kwa ufupi kuhusiana na kampuni
hiyo wakati wa mjadala kuhusu fikra za kibunifu kwa ajili ya kuinua
uchumi kwa wanafunzi wa elimu ya juu leo jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akiwa katika picha ya pamoja na
baadhi ya washiriki wa mjadala kuhusu fikra za kibunifu kwa ajili ya
kuinua uchumi kwa wanafunzi wa elimu ya juu leo jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Genofeva Matemu – MAELEZO
Na Frank Shija – MAELEZO
Vijana
wamehasishwa kuwa wabunifu ili kujiletea maendeleo yao badala ya
kusubiri kuajiriwa mara wanapomaliza masomo ya elimu ya juu.
Rai
hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel
alipokuwa akiwasilisha mada kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaosoma
masomo ya Sayansi kutoka vyuo mbalimbali kuhusu fikra za kibunifu kwa
ajili ya kuinua uchumi leo jijini Dar es Salaam.
Aidha
Prof. Gabriel amewataka vijana kuwa wabunifu ili kwenda na wakati ikiwa
ni njia ya kukabiliana na changamoto na kasi ya mabadiliko ya
kiteknolojia ambapo kila siku mambo yanabadilika kuendana na wakati.
“Pamoja
na changamoto nyingi vijana mnapaswa kuwa wabunifu kwani ubunifu ndio
njia pekee ya kushindana katika biashara na kuweza kukabiliana na kasi
ya mabadiliko ya teknolojia katika maendeleo”, Amesema Prof. Gabriel.
Mkurugenzi
huyo ameongeza kuwa vijana wengi wamekosa uthubutu wa kujihusisha na
ajira binafsi na kusababisha ongezeko la watu wasiokuwa na ajira kwani
kwa sasa takwimu zinaonyesha kuwa kuna vijana takribani 16,195,370
nchini. Idadi hii ni sawa na 35.1% ambapo kati ya hao13.4% hawana
ajira.
Kwa
upande wake Mwakilishi wa Kampuni ya Sparke International
inayojihusisha na bishara za kiwanda cha utengenezaji wa nguo, Bwana
Gerald Reuben ambaye pia ni mwanafunzi wa elimu ya juu amesema kuwa wao
kama vijana wamethubutu kujiajiri wenyewe na wanataraji kuajiri vijana
wengi zaidi.
Reuben
amesema kuwa Kampuni yao inatokana na muunganiko wa vijana kutoka Chuo
Kikuu Cha Dodoma kuunganisha mawazo na kuanzisha Kampuni hiyo ambayo
itasaidi wakulima wa zao la Pamba kuingia katika soko la ndani.
0 comments:
Post a Comment