|
|
Rais
wa chama cha soka nchini Ghana Kwesi Nyantakyi amethibitisha kuwa
mchezaji wao Kevin Prince Boateng ameomba kurejea timu ya taifa ya nchi
hiyo maarufu kama Black Stars.
Mchezaji
huyo wa AC Milan ya Italia alitangaza kujiweka kando na timu ya taifa
ya Ghana mara baada ya kumalizika kwa fainali za kombe la dunia nchini
Afrika Kusini mwaka 2010.
Rais
wa soka wa Ghana amesema kurejea kwa mchezaji huyo kwa kikosi cha taifa
itakuwa faraja kubwa kwani amesema yuko fiti kwa ajili ya mechi
mbalimbali zinazoikabili timu hiyo.
Watoto wa Pele nao warejea kikosini Black Stars
Andre
na Jordan Ayew kwa pamoja wamekubali kurejea nyumbani baada ya kufanya
mashauriano na rais wa Ghana John Mahama mjini Accra.
Ndugu
hao wawili walitangaza kuwa hawataichezea tena timu ya taifa ya Ghana
mwezi Februari, baada ya kutofautiana na wasimamizi wa timu hiyo ya
taifa ya Black Stars.Ripoti zinasema wachezaji hao wawili wa klabu ya Marseille ya Ufaransa walifanya mazungumzo na rais Mahama wakati alipokuwa ziarani nchini Ufaransa.
Na katika mkutano wao wa pili, hii leo wachezaji hao waliafikiana kurejea tena nyumbani ili kuichezea Black Stars.
0 comments:
Post a Comment