Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kocha mtarajiwa wa klabu ya Manchester City Manuel Pellegrini amekutana na mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Txiki Begiristain pamoja na mkurugenzi mkuu Ferran
Soriano ili kuweka sawa baadhi ya mambo kabla ya kutangazwa rasmi
kurithi mikoba ya kocha aliyetimuliwa klabuni hapo Roberto Mancini.
City
wanatarajiwa leo hii au kesho kumtangaza Pellegrini kuwa bosi mpya wa
miamba hiyo ya soka nchini England baada ya kukubaliana ana kocha huyo
wa zamani wa klabu za Malaga na Villarreal za nchini Hispania.
Usiku
wa jana, City walithibitisha kumsainisha mkataba winga machachari wa
Sevulla, Jesus Navas kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 14.9
Baada
ya kusaini City, Navas mwenye umri wa miaka 27 alisema ” Manchester
City ni timu inayonifurahisha sana, nafikiri ni wakati wangu muafaka
kuifanyia makubwa”.
Kocha
mpya wa City, Pellegrini anatarajiwa kufanya mazungumzo na wachezaji
Carlos Tevez, Gareth Barry na Joleon Lescott ili kuwasajili kwa ajili ya
msimu ujao.
City
watasafiri kwenda Afrika kusini, Hong Kong na Helsinki kujiandaa na
msimu mpya wa ligi kuu nchini England pamoja na michuano mingine barani
Ulaya.
Bosi Mpya: Manuel Pellegrini anatarajiwa kujiunga na City siku chache zijazo
Mashine
mpya: Jesus Navas (juu) na Fernandinho (chini) tayari wameshajiunga na
klabu ya Manchester City kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu nchini
England
0 comments:
Post a Comment