Thursday, June 6, 2013

47091_ori_stefano_mwasika
Na Baraka Mpenja
Mlinzi wa kushoto wa klabu ya Yanga ya Dar es salaam, Stephano Mwasyika amekiri kumalizika kwa mkataba na mabingwa hao wa ligi kuu msimu uliopita na kombe la Kagame , na kukiri kutokusaini mkataba mpya wa kuwatumikia wanajangwani hao msimu ujao.
Mwasyika ameimabia MATUKIO DUNIANI kuwa anamshukuru mungu kumaliza mkata na Yanga kwani ameishi kigumu sana hasa msimu uliopita kutokana na kutoelewana na baadhi ya viongozi wa klabu hiyo.
“Kwasasa wanajangwani nimemalizana nao, sifikirii hata kidogo kuongeza mkataba, mpira ni kazi yangu, lakini kwa Yanga mimi basi, acha niangalie mambo mengine”. Alisema Mwasyika.
Akiongelea maisha yake ya baadaye, Mwasyika amesema kuna timu kadhaa za hapa Tanzania ambazo anafanya nazo mazungumzo, lakini kwa sasa hayuko tayari kutaja timu hizo.
“Msimu ujao nitacheza ligi ya hapa nyumbani, kama watatokea mawakala wa kunitafutia timu nje ya nchi basi nitaenda, lakini bado nitakuwepo msimu ujao. Timu mpya ambayo nitaichezea nitataja hapo baadaye”. Alisema Mwasyika.
Mwasyika alisema kuwa wachezaji wengi wanatamani kucheza Yanga na Simba ambazo zina presha kubwa ya mashabiki, lakini yeye ameona hali halisi ya klabu hizo, hivyo anatamani kutoka kwenda timu nyingine ili akacheze soka la uhakika.
“Mara nyingi timu kubwa zina fitina sana, kwa upande wangu siogopi kitu, hata ikitokea penati naenda kupiga kama kawaida, lakini kwa ukweli watu wengi wanaogopa sana kutokana na majungu ya watu”.
Kwa wanaofuatilia mechi za Simba na Yanga, endapo timu itapata penati, wachezaji wengi wanakimbilia kunya maji, lakini ukweli ni kwamba wanafanya vile kukwepa lawama za mashabiki na viongozi.
“Watu wanazuga tu, hakuna cha kunywa maji, ni uoga wa kupiaga penati, lakini mimi katika maisha yangu siogopi, huwa napiga tu na sijawahi kukosa penati”. Alijisifu Mwasyika.
Akizungumzia msimu uliopita wa ligi kuu Tanzania bara, Mwasyika alisema ushindani ulikuwa mkubwa ambapo amezitaja klabu za Kagera Sugar, Coastal Union, Ruvu Shooting, kuonesha kandanda safi zaidi.
“Kuna timu nyingi sana zinazofanya vizuri kwa sasa, lakini Coastal na Ruvu zilicheza vizuri sana, nao Tanzania Prisons walijituma sana licha ya kuathiriwa na ajali, pia Kagera walicheza vizuri sana”. Alisema Mwasyika.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video