Na Baraka Mpenja
JANA
kulikuwa na Mechi kadhaa za Makundi Barani Afrika kusaka Timu 5
zitakazocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014 na
zifuatazo ni taarifa fupi ya baadhi ya Mechi hizo.
Morocco 2 Gambia 0
Morocco
Jana waliipikua Tanzania Nafasi ya Pili ya KUNDI C baada ya kuichapa
Timu ya mkiani Gambia kwa Bao 2-0 katika Mechi iliyochezwa huko
Marrakech.
Bao za Morocco zilifungwa na Barrada na Younes Belhanda.
Katika
KUNDI C, ambalo leo, Tanzania inaikaribisha Ivory Coast Jijini Dar es
Salaam, Ivory Coast ndio Vinara wakiwa na Pointi 10, Morocco 8, Tanzania
6 na Gambia 1.
Uganda 2 Angola 1
STRAIKA
wa Uganda, Emmanel Okwi Jana aliifungia Uganda Bao muhimu katika Mechi
yao ya KUNDI J la kuwania kwenda Brazil Mwaka 2014 kucheza Fainali za
Kombe la Dunia walipoifunga Angola Bao 2-1 na kutwaa uongozi wa Kundi
hilo.
Katika
Mechi hiyo, Angola walitangulia kufunga kupitia Job lakini Uganda
walipiga Bao 2 Wafungaji wakiwa Emmanuel Okw na Tonny Mawejje.
Ushindi huo umewafanya Uganda wawe juu ya Senegal kwa Pointi 2 na leo huko Monrovia Lineria itacheza na Senegal.
Congo 0 Burkina Faso 1
Kwenye
KUNDI E, waliokuwa Vinara, Congo wakiwa Nyumbani Pointe Noire,
walijikuta wakipoteza uongozi huo kwa kuchapwa Bao 1-0 na Burkina Faso
kwa Bao la Aristide Bance na sasa Burkina Faso wako kileleni Pointi 2
mbele ya Congo.
Burkina Faso ndio walimaliza wa pili nyuma ya Mabingwa Nigeria kwenye AFCON 2013.
Katika
Mechi nyingine ya KUNDI E, Hetitriki ya Pierre-Emerick Aubameyang
iliwapa ushindi wa Bao 4-1 Gabon dhidi ya Niger na kuwa Pointi 2 nyuma
ya Vinara Burkina Faso.
Zambia 1 Sudan 1
Wakiwa kwao, Zambia jana walibanwa na kutoka Sare ya Bao 1-1 na Sudan ambayo haina matumaini ya kusonga mbele.
Matokeo
hayo yamewafanya leo Ghana, ambao wako Ugenini kucheza na Lesotho, kuwa
na nafasi murua kutwaa uongozi wa KUNDI D ikiwa watashinda na kujiweka
kwenye hali nzuri kucheza na Zambia huko Accra katika Mechi yao ya
mwisho ya Kundi.
0 comments:
Post a Comment