Mfaransa, Patrick Liewig (kulia) akizungumza na msaidizi wake Jamhuri Kiwhelu “Julio”
Na Baraka Mpenja
Aliyekuwa
kocha wa wekundu wa msimbazi Simba, Mfaransa Patrick Liewig ameendelea
kusisitiza nia yake ya kuwaburuza Simba mahakamani endapo watapuuzia
haki yake ya msingi katika mkataba wake na klabu hiyo.
Katika mahojiano maalumu, Liewig ameimbia MATUKIO DUNIANI kuwa anaheshimu sana maamuzi ya Simba kumuachisha kazi yake ya kukinoa
kikosi chake, lakini nao waheshimu makubaliano ya mkataba wake ambao
unaisha mwakani mwezi wa sita.
“Mimi
sikuambiwa kama nimefukuzwa bali niliambiwa nikapumzike, nimerudi
kuifundisha timu yangu kujiandaa na Kombe la Kagame, nimekuja na mipango
yangu ya mazaoezi, nafika nakuta Simba wameajiri kocha mpya, sawa
naheshimu maamuzi yao lakini nao waheshimu mkataba”. Alisema Liewig.
Kocha
huyo aliyemaliza ligi akiwa nafasi ya tatu katika msimamo na mbaya
zaidi akafungwa na Ynaga mabao 2-0 mechi ya mwisho ya ligi kuu soka
Tanzania bara mei 18 mwaka huu, amesisitiza kuwa yeye anajitambua kuwa
ni kocha wa simba na ana mkataba ambao unaisha mwezi juni mwakani, na
kama Simba wameamua kuuvunja sawa, lakini wanatakiwa kumlipa madai yake
ili atimke zake nchini.
“Mimi
nashangaa sana, kwanini wasingeniambia mapema kuwa hawanitaki, naipenda
kazi yangu na mimi ni kocha wa kimataifa, wachezaji walikuwa
wanashindwa kunielewa mwanzoni, lakini ikafika wakati wakanipatia
vizuri, nimekuja kuisaidia timu halafu nakutana na hali hii, imenichosha
sana.” Alisema Liewig.
Liewig
maarufu kama “Babu” alisisitiza kuwa kwa sasa anawasiliana na
mwanasheria wake ili kudai haki zake za msingi, na kamwe Simba
wasijisumbue kwani lazima wamlipe madai yake ya mkataba.
Kwa sasa kocha Abdalaah Kibadeni “King Mputa” amerithi mikoba ya Liewig na tayari ameshaanza kazi rasmi Msimbazi.
MATUKIO DUNIAN
ilihitaji kujua kama Liewig anaweza kufundisha timu nyingine ya soka
nchini Tanzania endapo akipata nafasi, na ndipo alipojibu kuwa anaweza
kufundisha, lakini akasema timu anazoweza kufundisha ni Azam fc au
Yanga.
“Naweza
kufundisha timu nyingine kama Azam na Yanga, lakini sidhani kama naweza
kupata nafasi kwani tayari Yanga ni mabingwa na wanamuamini kocha wao,
hali kadhalika Azam fc wanaendelea vizuri na kocha wao, hivyo sina imani
ya kupata nafasi katika timu hizo”.Alisema Liewig.
Kocha
huyo aliongeza kuw amefurahi kuwaona vijana wake wakiendelea vizuri
katika kikosi cha Taifa Stars ambapo alifurahi zaidi kumuona adui yake
Mwinyi kazimoto Mwitula akipasha misuli katika kikosi cha stars.
“Nimefurahi
kumuona Mwinyi, tuligombana sana na mimi, kama nisingefanya vile
usingekuwepo hapa leo hii, nimefurahi amekuja kunisalimia, nampenda
sana”. Alisema Liewig.
Akizungumzia
mchezo wa leo katika ya taifa stars dhidi ya Ivory Coast, Liewig
amesema Taifa stars wanaweza kupata ushindi kama wachezaji watajituma na
kusikiliza maelezo ya mwalimu.
Kocha huyo alisema Ivory coast anawafahamu vizuri na wana wachezaji bora zaidi, lakini katika soka wanaweza kufungwa vizuri tu.
0 comments:
Post a Comment