Saturday, June 8, 2013

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Katika harakati zake za kuimarisha kikosi cha washika bunduki wa London, Kocha wa klabu hiyo, Mfaransa Arsene Wenger amesema timu hiyo inaendelea na mazungumzo ya kina na nyota wa Real Madrid ya Hispania Gonzalo Higuain ili kuinasa saini ya mshambuliaji huyo kwa ada ya uhamisho wa pauni milioni 20.
The Gunner hawana imani ya kumpata Stevan Jovetic baada ya Chelsea kuonesha nia ya kumsajili kwa kitita cha kutosha, sasa hesabu zao ni kwa Higuain ambaye pia anawaniwa  na miamba ya soka la Italia, Juventus.
Wakati Wenger akihaha katika usajili, bado ndoto yake kubwa ni kumpata nyota wa mashetani wekundu, Machester United, Wayne Roooney ambapo amekubali kuvunja benki ili kumnasa nyota huyo aliyeonesha nia ya kutaka kuihama United.
Wakati Mfaransa huyo akitanga na ya kumtaka Higuain, nyota huyo amekiri kupenda kuhamia Emirates endapo watamlipa kile anachokihitaji.
Higuain mwenye umri wa miaka 25 kwa sasa, akiwa Real Madrid anavuta mkwanja wa pauni laki mbili na elfu thelathini kwa wiki, pesa ambayo ipo chini ya uwezo wa Arsenal.
London calling: Gonzalo Higuain (centre) is a top target for Arsenal boss Arsene WengerLondon inamuita: Gonzalo Higuain (katikati) yupo katika rada za bosi wa Arsenal, mzee Arsene Wenger
Top target: Stevan Jovetic (left) is wanted by several Premier League clubs this summerHuyu ndio kila kitu: Stevan Jovetic (kuahoto) anawindwa na timu nyingi za ligi kuu nchini Uingereza
Wakati huo huo Marseille wanamtaka mshambuliaji wa Arsenal, Gervinho kwa mkopo. Huku Barcelona wakimhitaji beki wa Arsenal Thomas Vermaelen.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video