Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Mikakati
ya Cristiano Ronaldo kurejea Ligi Kuu ya England katika klabu ya
Manchester United imepata nguvu tena baada ya mchezaji huyo mwenye
thamani ya Pauni Milioni 80 kukanusha taarifa za kusaini Mkataba mpya
Real Madrid ya Hispania .
Baadhi
ya Mashabiki wa klabu ya Manchester United nchini England walijaribu
kuchangishana kiasi kikubwa cha fedha ili kumrejesha nyota huyo wa
kimataifa wa Ureno lakini Uongozi wa Old Trafford ukasema ni kinyume cha
taratibu mashabiki kutoa fedha mfukoni na kumnunua mchezaji.
Sehemu
ya taarifa hiyo ilidokeza kuwa kocha ndiye mwenye kuamua mchezaji gani
anahitaji na klabu ya Man United haijafilisika kiasi cha kuwalazimu
mashabiki kuchangisha fedha bali wanasubiri mapendekezo ya kocha David
Moyes anahitaji wachezaji gani.
Manchester
United inajiamini itamsajili tena mshambuliaji huyo mwenye umri wa
miaka 28, Ronaldo kabla ya taarifa kutolewa kwa umma na Rais Florentino
Perez wa Real Madrid ya Hispania kwamba Ronaldo yuko tayari kusaini
Mkataba mpya kubaki Bernabeu kwa kipindi chake chote kilichobaki kwenye
soka.
Marafiki wakubwa: Alex Ferguson na Cristiano Ronaldo baada ya kutwaa ubingwa wa ligi ya mabingwa barani ualya dhidi ya Chelsea
Daima United: Hawa jamaa wanaweza kukutana tena Old Traford misimu ijao
Ronaldo na Ferguson mara zote wana mahusiano mazuri sana
0 comments:
Post a Comment