Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kiungo
wa zamani na nahodha wa washika bunduki wa London, Asernal na sasa
anakipa kwa miamba ya soka nchini Hispania, FC Barcelona, Cesc Fabregas
leo hii amevunja ukimya na kusema kuwa anataka kukaa katika klabu yake
hiyo labda Barca wamuuze wenyewe.
Fabregas
ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kusambaa taarifa kuwa nyota huyo
anataka kurudi ligi kuu nchini England huku United wakionekana kumuweka
katika rada zao.
Fabregas
tangu ajiunge na klabu ya Barcelona mnamo mwaka 2011, hajafurahia
maisha yake ya soka baada ya kukosa namba ya kudumu katika kiosim cha
kwanza cha miamba hiyo ya soka duniani.
Mtandao
wa Fullshangwe kwa msaada wa Sportsmail.com unatambua kuwa Febregas
ameshaeleza nia yake ya kurudi ligi kuu soka nchini England, huku
akitajwa kujiunga na mabingwa hao manchester United.
Lakini
leo hii mchana nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 ameibuka tena na
kusema kuwa anataka kubaki katika klabu hiyo aliyoanzia kucheza soka.
“Kama
Barcelona watasema hawanitaki mimi, basi ni kitu kingine, lakini
kiukweli nataka kushinda mataji mengi zaidi nikiwa Camp Nou. Hii ndio
ndoto yangu tangu nikiwa mtoto mdogo”. Alisema Fabregas.
Fabregas
alisisitiza kuwa kama watu watakuwa wanamzomea, itabidi akubaliane na
hali halisi kwani ndio maisha ya soka, kuna wakati mambo yanakwenda
vizuri na kuna wakati mambo yanakwenda vibaya.
Cesc
Fabregas amefunguka na kusema kuwa anataka kupambana Camp Nou mpaka
kieleweke, hataki kuondoka ingawa anahusishwa na kuhamia ligi kuu nchini
England. Pichani juu alikuwa anapambana na vijana wa Azzuri, timu ya
taifa ya Italia.
0 comments:
Post a Comment